Tuesday, February 28, 2012

Kwa Nini Waislamu Wamegawanyika?


Kwa Nini Waislamu Wamegawanyika Katika Makundi Tofauti Ya kuelewa Dini Yao?


Raashid Bin Husayn
Wakati Waislamu wote wanamfuata Mtume mmoja na Qur-aan moja lakini kuna makundi mengi na tofauti yaliyogawanyika miongoni mwa Waislamu?

1.    WAISLAMU NI LAZIMA WAUNGANE
Ukweli ni kwamba Waislamu wa zama hizi, wamegawanyika mapote tofauti. Kugawanyika huko hakuungwi mkono na Uislamu kabisa. Uislamu unaamini ya kwamba wauumini ni lazima waungane.
Kwani Qur-aan Tukufu inasema:
"Na shikamaneni kwa kamba ya Mwenyezi Mungu nyote pamoja, wala msifarikiane. Na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu iliyo juu yenu: vile mlivyokuwa nyinyi kwa nyinyi maadui naye Akaziunganisha nyoyo zenu; kwa neema Yake mkawa ndugu. Na mlikuwa ukingoni mwa shimo la moto, Naye Akakuokoeni nalo. Namna hivi Mwenyezi Mungu Anakubainishia ishara Zake ili mpate kuongoka".
Qur-aan inasema pia:
"Enyi mlioamini! mtiini Mwenyezi Mungu na mtíini Mtume na wenye madaraka katika nyinyi. Na mkizozana katika jambo basi lirudisheni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume, ikiwa mnamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Hayo ndio bora zaidi na ndio yenye mwisho mwema.”


Waislamu wote ni lazima kushikamana na Kitabu na Sunnah sahihi na sio kugawanyika makundi makundi.


2.    IMEKATAZWA KUGAWANYIKA NA KUFANYA MAKUNDI

Mwenyezi Mungu Anasema ndani ya Qur-aan:

"Hakika walio igawa dini yao wakawa makundi makundi, huna uhusiano nao wowote. Bila ya shaka shauri yao iko kwa Mwenyezi Mungu; kisha atawaambia yale waliyokuwa wakiyatenda". [6:159]

Kwenye Aayah hii Mwenyezi Mungu Anasema ya kwamba yeyote yule asishirikiane na yule aliyeigawa dini yake katika makundi.
Lakini mtu akimuuliza Muislamu, ‘Wewe ni kundi gani?’, jibu litakuwa ‘Mimi ni Sunni’, au ‘Mie ni Ibadhi’. Na katika Masuni wengine hujiita Hanafi au Ash-Shaafi’iy au Maalik au Hanbaliy. Na humo tena utakuta mtu anajiita ‘Mimi Qadiriya’, ‘Mimi Naqshabandiya’ au ‘Mimi Shadhiliya’!


3.    MTUME (SWALLA ALLAAHU ‘ALAYHI WA SALLAM) ALIKUA MUISLAMU

Anaweza kuulizwa Muislamu, "kipenzi chetu Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) alikuwa nani? Alikuwa Ibadhi, Hanafi, au Ash-Shaafi’iy, au Hanbali au Maaliki? Jibu litakuwa hapana alikuwa Muislamu kama vile Manabii na Mitume ya Allaah (Subhaanahu wa Taa'ala) kabla yake.
Imesemwa kwenye sura ya 3 Aayah ya 52 ya kwamba ‘Iysa (‘Alayhis Salaam) alikuwa     ni Muislamu.
Hata ukiangalia,kwenye sura ya 3 Aayah ya 67 ndani ya Qur-aan ya kwamba Ibraahiym (‘Alayhis Salaam) hakuwa Myahudi wala Mnaswara lakini alikuwa Muislamu.

4.    QUR-AAN INATUAMRISHA TUJIITE WAISLAMU
Asiyekuwa Muislamu akimuuliza Muislamu wewe ni nani, bila ya shaka atasema 'mimi ni MUISLAMU", sio Hanafi au Ash-Shaafi’iy...

Jawabu hili linapatikana ndani ya Qur-aan katika Surah Fusswilat 41 Aayah ya 33 ambayo inasema:
"Na ni nani mbora wa kusema kuliko aitaye kwa Mwenyezi Mungu na akatenda mema, na akasema: Hakika mimi ni katika Waislamu"?

 Qur-aan inasema:
"Hakika mimi ni katika Waislamu".Kwa maana nyengine inasema "mimi ni Muislamu".

Mtume 
(Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) aliandika barua kwa mfalme na mtawala ambaye alikuwa si Muislamu kumtaka awe Muislamu. Kwenye barua hiyo kulikuwemo  na Aayah ya Qur-aan iliyoko katika Surah ya 3 Aal-‘Iimraan Aayah ya 64 isemayo:
"Shuhudieni ya kwamba mimi ni Muislamu"
  
5.    NI WAJIBU KUWAHESHIMU WANAZUONI [MAULAMAA] WA KIISLAMU
Ni lazima kuwaheshimu wanazuoni wakubwa wa Kiislamu wakiwemo maImam wakubwa Imam Abu Haniyfah, Imam Ash-Shaafi’iy, Imam Ahmad bin Hanbali na Imam Maalik [Allaah Awarehemu].
Walikuwa ni wanazuoni wakubwa twamuomba Mwenyezi Mungu Awalipe ujira wao kwa utafiti wao na kazi ngumu waliyoifanya.
Hakuna kipingamizi kama kila mmoja wetu atakubaliana na utafiti wa Imam Abu Haniyfah au wa Imam Ash-Shafi’iy na wengineo. Lakini linapoulizwa swali "wewe ni madhehebu gani?" Jibu liwe "mimi ni Muislamu".

Zifuatazo ni kauli za Maimam juu ya msimamo wao wakufuata mwenendo sahihi yaani kitabu na Sunnah sahihi.

Imam Abu Haniyfah [Allaah Amrehemu] anasema:
"Itakaposihi Hadithi basi ndio madhehebu yangu". [Al-Haashiyah Juzuu ya 1 uk.63]
Imam Maalik [Allaah Amrehemu] anasema:
Hakuna yeyote baada ya Mtume isipokua kauli yake huchukuliwa na kuachwa". [Irshaadus Saalik juzuu ya 1 uk. 227]

Imam Ash-Shaafi’iy [Allaah Amrehemu] amesema:
"Itakaposihi Hadithi basi ndio madhehebu yangu" [Al Majmuu Al Mussawwiy Juzuu ya 1 uk 63]

Baadhi  wanaweza kujadili kwa kunukuu hadithi ya kipenzi chetu Mtume 
(Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) kutoka kwenye Sunan Abu Daawuud hadithi nambari 4579, kwenye hadithi hii mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa  sallam) iliripotiwa ya kwamba alisema:
"Umati wangu utagawanyika ktk makundi 73"
Hadithi hii inaripoti ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) aliashiria ya kwamba umati wake utagawanyika makundi sabiini na tatu, hakusema Waislamu wawe katika harakati za kujigawanya katika makundi. Qur-aan Tukufu inatuamrisha tusiunde makundi. Wale wanaofuata muongozo wa Qur-aan na Sunnah Sahihi za Mtume wetu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) na wasiounda makundi wao ndio walio katika mfumo sahihi.
Kulingana na At-Tirmidhiy hadithi nambari 171, Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) iliripotiwa ya kwamba alisema:
“Ummah wangu utagawanyika katika mapote 73, na yote motoni isipokuwa kundi moja tu." Maswahaba waliuliza: ‘Ni lipi hilo, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?’ Akasema: (Ni lile nililokuwemo mimi na swahaba zangu).”

Aayah nyingi ndani ya Qur-aan zimeamrisha kwa kusema "Mtiini Allaah na mtiini Mtume".
Muumini wa kweli ni lazima afuate Qur-aan na Sunnah (Hadithi) Sahihi.
Anaweza mtu kukubaliana na ‘Aalim yeyote yule ilimuradi yuko kwenye mfumo wa mafundisho yatokanayo na Qur-aan na Sunnah Sahihi. Ikiwa mafundisho yatakwenda kinyume na maneno ya Allaah (Qur-aan) au na Sunnah za Mtume Wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam), hivyo mafundisho hayo hayatakuwa na uzito wowote bila ya kuzingatia ya kwamba ‘Aalim (mwanachuoni) huyo alikuwa mwanachuoni mkubwa au la.

6.    UMUHIMU WA KUHITAJI REHMA ZA ALLAAH (SUBHAANAHU WA TA’ALA)
Kuna baadhi ya watu wanajaribu kutoa hoja ya kwamba mbona Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) alishasema ndani ya Qur-aan ya kwamba:

“Na Mola wako Angelipenda Angewafanya watu wote wakawa umma mmoja. Lakini hawaachi kukhitalifiana” [Surat Huud 3:118]

Ni kweli aya hii ndio lakini walisahau Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kwenye Aayah inayofuata aliwavua baadhi ya watu kwa kusema ila wale aliowarehemu.
Kama ilivyosema:

“Isipokuwa wale ambao Mola wako Amewarehemu; na kwa hiyo ndio Mwenyezi Mungu Amewaumba. Na litatimia neno la Mola wako: Kweli kweli nitaijaza Jahannam kwa majini na watu pamoja.” [Surat Huud 3: 119]

a. Kuhitaji Rehma za Allaah ni Muhimu na hili limedhibitishwa na Mtume wetu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa  sallam) kwenye hadithi pale aliposema ya kwamba:
"Hataingia yeyote yule peponi ila kwa rahma ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Maswahaba wakamuuliza, hata wewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Akajibu hata mie ila kwa rahma za Allaah."

b. Hata Nabii Yuusuf (‘Alayhis Salaam) alipojaribiwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)  kwa wanawake kumtaka na alipofaulu mtihani huo na kuulizwa ni kitu gani kilikufanya ukafaulu mtihani huu?
Alijibu ifuatavyo kama Qur-aani inavyosema:
“Nami sijitoi lawamani. Kwa hakika nafsi ni mno kuamrisha maovu, isipokuwa ile ambayo Mola wangu Aliyoirehemu. Hakika Mola wangu ni Msamehevu na Mwenye kurehemu.” [Surat Yuusuf 12: 53]

Hivyo tunaona ya kwamba rehma za Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) tunazihitaji kama walivyozihitaji Mitume na Manabii waliopita.



HITIMISHO
Iwapo Waislamu wote watasoma Qur-aan kwa kuielewa, kuzingatia yaliyomo ndani yake na kushikamana na Sunnah Sahihi na kutaraji rehma za Allaah (Subhanaahu wa Ta'ala) basi tofauti nyingi (au hayo makundi yalioko yatafutika) na kutapatikana ufumbuzi na tutakuwa ummah mmoja inshaAllaah.

Jesus predicted Mohammad (SAW) in older bible in Turkey


Jesus Foresaw Prophet Mohammad's Arrival in Old Bible Found in Turkey

Turkish culture and tourism minister says Vatican has asked to see the book

A 1,500-year-old Bible in which Jesus is believed to have foretold the coming of the Prophet Mohammed to Earth has attracted attention from the Vatican this week.

Pope Benedict XVI has reportedly requested to see the book, which has been hidden in Turkey for the last 12 years, according to the Daily Mail.

The text, reportedly worth $22 million, is said to contain Jesus’ prediction of the Prophet’s coming but was suppressed by the Christian Church for years for its strong resemblance to the Islamic view of Jesus, Turkish culture and tourism minister Ertugrul Gunay told the newspaper.
“In line with Islamic belief, the Gospel treats Jesus as a human being and not a God. It rejects the ideas of the Holy Trinity and the Crucifixion and reveals that Jesus predicted the coming of the Prophet Mohammed,” the newspaper reported.

“In one version of the gospel, he is said to have told a priest: ‘How shall the Messiah be called? Mohammed is his blessed name.’

“And in another, Jesus denied being the Messiah, claiming that he or she would be Ishmaelite, the term used for an Arab,” the newspaper added.

According to the report, Muslims claim the text, which many say is the Gospel of Barnabas, is an addition to the original gospels of Mark, Matthew, Luke and John.

St. Barnabas is traditionally identified as the founder of the Cypriot Church, an early Christian later named an apostle.

Gunay said the Vatican has officially requested to see the book, which Turkey had discovered during a police anti-smuggling operation in 2000.

The gang was reportedly convicted of smuggling various items seized during the operation, including the Bible, and all the artifacts were kept in a safe at an Ankara courthouse.

It remained closely guarded by authorities before being handed over to the Ankara Ethnography Museum where it will soon be put on show.

A photocopy of a single page from the leather-bound, gold-lettered book, penned in Jesus’ native Aramaic language is reportedly worth about $2.4 million.

But skepticism over the authenticity of the ancient handwritten manuscript has arisen.

Protestant pastor İhsan Özbek has said this version of the book is said to come from the fifth or sixth century, while St. Barnabas had lived in the first century as one of the Apostles of Jesus.

“The copy in Ankara might have been written by one of the followers of St. Barnabas,” he told the Today Zaman newspaper.

“Since there is around 500 years in between St. Barnabas and the writing of the Bible copy, Muslims may be disappointed to see that this copy does not include things they would like to see … It might have no relation with the content of the Gospel of Barnabas,” Özbek added.

But suspicions could soon be laid to rest.

The real age of the Bible could soon be determined by a scientific scan, theology professor Ömer Faruk Harman told the Daily Mail, possibly clarifying whether it was written by St. Barnabas or a follower of his.
By Eman El-Shenawi

Tahadhari ya Tanzania na Al Shabbab

Kamati ya Kutetea Haki za Waislamu nchini, imeihadharisha Serikali kutojihusisha na mambo ya kidini hasa yanayohusu kundi la Al-shaabab kwa shinikizo la mataifa makubwa.

Katibu wa kamati hiyo, Shekhe Ponda Issa Ponda, aliyasema hayo Dar es Salaam mbele ya waandishi wa habari.

Alisema kamati hiyo imemwandikia barua Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha, kupinga kauli yake aliyowataka Watanzania kuwa makini na wahamiaji haramu ili kudhibiti kundi hilo lisiingie nchini.

Shekhe Ponda alisema ni vyema Serikali ikawa makini na sera za mataifa makubwa ambayo yameingia katika migogoro na baadhi ya nchi za Afrika kwa maslahi binafsi, “Serikali iache kujiingiza katika migogoro na kundi hili, jambo la msingi ni kuimarisha ulinzi wa mipaka yetu si vinginevyo,” alisema Shekhe Ponda na kuongeza kuwa, si kweli kwamba kundi hilo ni la kigaidi kama alivyosema Nahodha bali kinachofanywa na kundi hilo ni kulinda mipaka ya nchi yao.

Alisema Nahodha hapaswi kuwaweka Watanzania katika hofu ya kuvamiwa na kushindwa kusafiri kwa shughuli mbalimbali ambazo ndioz huwapatia kipato na kukuza uchumi wao kutokana na taarifa za upotoshwaji dhidi ya kundi hilo, “Waziri anapozungumzia kundi hili ni sawa na kudhalilisha Uislamu, mbona hivi karibuni wameingia Wakongo wakiwa na silaha nzito lakini Serikali haikufanya kitu, kwanini Al-Shaabab,” alihoji Shekhe Ponda.

Ponda alisema kauli iliyotoa Nahodha, imelenga kuwagawa Watanzania ili waichukie nchi ya Somalia kitu ambacho si sahihi.

Hivi karibuni, Waziri Nahodha alisema kutokana na nchi jirani ya Kenya kukumbwa na vitendo vya uhalifu vinavyofanywa na kundi hilo, umefika wakati wa Watanzania kuwa makini na watu ambao wanaingia nchini kinyemela bila kufuata utaratibu.

taarifa via Majira
UPDATE ya tamko rasmi:
Bismillahir Rahmanir Rahiim
KUMB: KKHWT/WMN/1/011
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
S.L.B 2217 Dar es Salaam Tanzania.

YAH: TAHADHARI KWA TANZANIA KUTUMIWA NA MAREKANI DHIDI YA UISLAMU KATIKA SUALA AL-SHABAB
Ndugu Waziri Tarehe 16.11.2011 ulikutana na vyombo vya habari. Lengo ilikuwa ni serikali kutoa tahadhari ya uwezekano wa nchi kushambuliwa na wapiganaji wa Al-Shabab wa Somalia. Wiki tatu kabla, Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania naye alitoa tahadhari kama hizo. Katika suala la majeshi ya Kenya kuivamia Somalia Serikali ya Tanzania ilipongeza hatua hiyo.

Sababu zilizo tolewa na serikali katika tahadhari hiyo ni 5:
1. Al-Shabab ni magaidi.
2. Al-Shabab wameshambulia Kenya mara 3.
3. Watanzania wanadhaniwa kujiunga na Al-Shabab
4. Tanzania imekamata ‘wahamiaji haramu’ kutoka Somalia.
5. Al-Shabab wamesababisha ukosefu wa ajira Somalia na hatimaye vijana
wamechagua ugaidi kama ajira

UKWELI KUHUSU AL-SHABAB NA SOMALIA. Ndugu Waziri, Somalia ni nchi huru katika nchi za bara la Afrika.
Somalia ni nchi ya Waislamu kwa asilimi 99.
Kama zilivyo nchi nyingi duniani, imepita katika kipindi cha amani na vita.
Tafauti zinazoendelea Somalia ni tafauti za ndani na za kiutawala.

Somalia imekuwa na mpishano mkubwa wa utawala kama zilivyo nchi nyingine.Utawala ulio muhimu kwa muktadha wa sasa wa Somalia ni ule wa Rais Mohammed Siad Barre. Yeye aliongoza kwa kufuata siasa za mrengo wa magharibi mpaka alipoangushwa mwaka 1991. Utawala uliofuatia zilikua tawala za Koo. Tawala hizi ziliondolewa na Utawala wa Mahakama za Kiislamu. Utawala huu wa Kiislamu ambao uliripotiwa na mashirika ya kimataifa kurejesha amani kwa kiasi kikubwa katika maeneo kadhaa ya Somalia, ulidhoofishwa na mashambulizi ya majeshi ya uvamizi ya Marekani na Ethiopia. Ni kwa muktadha huo wapiganaji wa Somalia walijipanga upya kwa anuani ya Al-Shabab kulinda nchi yao dhidi ya uvamizi na kuendeleza utawala wa Kiislamu ulio asisiwa na Mahakama za Kiislamu.

UREJESHWAJI WA AMANI SOMALIAKatika hali inayoendelea Somalia, baadhi ya mataifa ya nje yalijipa jukumu la kuunda serikali mezani kwa kushirikiana na baadhi ya wasomali. Hatimaye serikali hiyo iliyoundwa nchini Kenya imepelekwa Somalia kwa msaada wa majeshi ya nchi hizo na kutangaza kuwa ndio serikali halali kwa wananchi. Matarajio yenye dhamira njema,yalikuwa ni kuona Umoja wa Afrika, Umoja wa Mataifa na wengineo wakiunga mkono amani iliyoanza kujitokeza Somalia chini ya Utawala wa Mahakama za Kiislamu.

Vilevile kupinga uvamizi wa Marekani na Ethiopia dhidi ya taifa huru. Matarajio mengine makubwa ilikuwa ni kuona mataifa na makundi yenye sifa ya uadilifu,yakielekea Somalia kutafuta amani kwa njia ya mazungumzo. Kigezo kikubwa kikiwa ni ridhaa ya wananchi walio wengi kwa mfumo wa utawala wanaoutaka wenyewe.

SIO HALALI KUIVAMIA SOMALIA. Somalia ni nchi huru ni dola ya wasomali wenyewe. Marekani bila ya ushahidi wa kisheria ndio walioanzisha propaganda za kuwahusisha mahasimu wao wakubwa Al-Qaida na Mahakama za Kiislamu na Al-Shabab nchini Somalia. Hatimaye Marekani ikaivamia kijeshi Somalia mpaka leo.

Katika hali ya kushangaza na inayo thibitisha ile dhana ya mataifa makubwa kufikiri kwa niaba ya mataifa ya Afrika, nchi za Burundi, Uganda, Ethiopia na hivi karibuni Kenya, nazo zimepeleka majeshi Somalia kwa tuhuma zile zile za Marekani. Mataifa hayo pia yanalazimisha kukubalika serikali iliyoundwa Kenya. Tanzania kwa upande wake ikijihusisha na mafunzo ya kijeshi kwa serikali iliyoundwa Kenya.

Ndugu Waziri jambo lingine la kuzingatia hapa ni kwamba, takriban nchi zote zilizo peleka majeshi Somalia, hazina amani katika nchi zao kutokana mashambulizi ya vikundi vinavyopinga serikali zao. Ajabu ya Mungu majeshi hayapelekwi katika nchi hizo kupambana na wapinzani wa serikali kama inavyofanywa kwa Somalia.
Ndugu Waziri, hatua hizi za Marekani na wapambe wake sio halali kwa kipimo chochote cha ukweli, utu, sheria, au hatua za kutafuta amani. Kwa muktadha huo utaona wasomali chini ya Al-Shabab wana kila sababu za kupambana na majeshi haya ya kigeni ima iwe ndani au nje ya Somalia na kufanya hivyo sio ugaidi bali ni hatua muhimu katika kulinda sio tu uhuru wa nchi yao bali uhuru wa Afrika nzima.

TANZANIA ISIJIINGIZE KIJESHI SOMALIA Pia isiwadhuru raia wake kwa propaganda za ugaidi.

Katika magereza yetu Tanzania wafungwa wana ‘vyeo’ visivyokuwa rasmi. Moja ya vyeo hivyo kinaitwa ‘kiherehere”. Huyu ni mfungwa ambaye ana tabia ya jambo lisilo muhusu kabisa lakini atajitahidi mpaka na yeye ahusike. Katika suala la Al-Shabab Tanzania inajitokeza kama ‘Kiherehere’.

Viongozi wa serikali ya Tanzania wanawashambulia Al-shabab bila hoja za msingi. Hoja za viongozi ni hizi zifuatazo: Al-Shababu ni magaidi, Al-Shabab wameshambulia Kenya,Watanzania wanadhaniwa kujiunga na Al-Shabab, Tanzania imekamata wahamiaji haramu kutoka Somalia, Al-Shabab wamesababisha ukosefu wa ajira Somalia na hatimae vijana wa wamechagua ugaidi kama ajira. Hoja hizi hazina mashiko.

Kwanini tupewe taarifa za wale tu wanaokwenda Somalia na sio kwengineko?. Na kama mtanzania shida yake imempeleka Somalia kujiunga na Al-Shabab iweje kosa liwe la Al-Shabab?.

Suala la nchi jirani kushambuliwa ni suala la ndani la nchi husika na aghlabu nchi zote tunazo pakana nazo zina matukio kama hayo. Mbona serikali ya Tanzania haijajitokeza kuvalia njuga mashambulizi ya kikundi cha Lord Resistance Arm kinacho uwa maelfu ya raia Uganda?. Mbona hatuja laani harakati za Mungiki wa Kenya?. Maimai wanapambana na serikali Kongo na huko Burundi na Rwanda nako kuna matukio kama hayo kila siku. Tanzania kama nchi inatakiwa kuimarisha ulinzi wa mipaka yake na matukio katika nchi jirani hayapaswi kubadilisha sera za ndani na nje ya nchi.

Hili la Tanzania kupokea wahamiaji wa kivita ni utaratibu wa kimataifa. Mwaka 2001, serikali ya Tanzania, ilipofanya mauwaji makubwa dhidi ya raia kule Pemba,Somalia kama nchi iliwapokea wakimbizi wa Tanzania. Wakimbizi hao mpaka leo wako Somalia wanatunzwa. Vipi wakimbizi wa Somalia wawe tishio kwa Tanzania na wakimbizi wa Tanzania wasiwe tishio kwa Somalia?. Katika kuthibitisha kuwa wakimbizi ni utaratibu wa kawaida, mwezi huu, Wakongo wakiwa na silaha za kivita wameingia na kupokelewa nchini mwetu. Ndio maana wananchi hawaja tahadharishwa wasiwasi wa nchi kuvamiwa na magaidi kutoka Kongo.

Ndugu Waziri, historia sahihi ya kuzaliwa Al-Shabab tumegusia huko nyuma. Suala la kukosekana kwa ajira kwa vijana wa Somalia hayo ni mambo ya kawaida kwa nchi maskini. Na kama ni kweli ulichosema, zingatia miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa ukosefu wa ajira kwa vijana ni Tanzania. Je ni sahihi kusema moja ya viashiria vya kutokea ugaidi Tanzania ni serikali kushindwa kukidhi ajira kwa vijana?.

Hoja nzito mnayoitoa katika kuwashambulia Al-Shabab ni ugaidi. Hivi kweli Tanzania mnao ushahidi wa kisheria unao thibitisha kuwa Al-Shabab ni magaidi?. Au bwana mkubwa Marekani akisema Al-shabab au kikundi fulani ni magaidi basi huo ni ushahidi tosha kwa Tanzania?. Hivi siku moja Marekani akiwageukia wakatangaza kuwa Chama kinachounda serikali CCM ni magaidi, mtakua na uso gani wa kuwaambia raia kuwa walichosema Marekani ni uongo?.

Ndugu Waziri kwa jinsi mlivyojitokeza katika suala hili wasiwasi wetu mkubw na huenda tayari Tanzania imeburuzwa na Marekani na sasa mnatafuta uhalali wa kupeleka rasmi majeshi Somalia. Tunatumia fursa hii kuwatahadharisha na kuwashauri muachane kabisa na agenda zinazoweza kuitumbukiza nchi katika
madhara makubwa yasiyokuwa ya lazima. Kama mmepeleka majeshi Somalia yarudisheni na kama hamjapeleka msipeleke. Aidha raia wasitiwe misukosuko kwa sababu tu ya kuwaridhisha wakubwa.

MSIMAMO WA WAISLAMU KUHUSU AL-SHABABHawa ni walinzi na wapiganaji wa Kiislamu walio tangaza wazi dhamira yao ya kulinda uhuru wao na kusimamisha mfumo wa utawala wa Kiislamu nchini mwao. Msimamo huu ni agizo la Qur’an Tukufu na historia inathibitisha Mtume wetu Muhammad (SAW) alitekeleza agizo hili kwa ufanisi mkubwa. Hatua yoyote ya kuwashambulia Waislamu wenye msimamo kama huu, hayo ni mashambulizi ya kiitikadi dhidi ya Uislamu na Waislamu wote duniani.

Serikali inapaswa kufahamu kuwa sehemu kubwa ya raia wa Tanzania ni Waislamu,tena wanao fahamu na kufuatilia kwa makini sera na siasa za ndani na nje za Tanzania.

Ndio maana tunawapa nasaha kwamba, kama ambavyo serikali ya Tanzania haikutangaza uadui na Rais Frederick Chiluba alipotangaza Zambia kuwa dola ya kikristo, na kama ambavyo haikutangaza uadui na kikundi cha Lord Resistance Arm kinachodai kutaka kusimamisha utawala wa Kikristo Uganda, na kama ambavyo haikutangaza uadui na Tume ya majeshi ya Kanisa nchini Tanzania, basi vile vile hapashwi kutangaza uadui na Waislamu wanaojitetea na kulinda utawala wa Kiislamu tena nchini Somalia.

SHERIA YA UGAIDI TANZANIA Ndugu Waziri utakumbuka mwaka 2002 Tanzania ilijadili muswada wa sheria iliyodaiwa ya kupambana na ugaidi. Bila shaka ulishuhudia upinzani mkali kutoka kwa makundi muhimu yakiwemo ya Waislamu, wanasiasa na wanasheria bobezi. Moja ya sababu zilizopelekea kupingwa kwa muswada huo ni kufanana kwa 99% na ule uliounda sheria ya ugaidi ya Marekani. Sheria ya ugaidi ya Marekani haina uhuru kwa watuhumiwa wala ukomo kwa watendaji wanapo shughulikia kinachoitwa ugaidi.

Muswada huo pia ulikuwa unashughulikia makosa na adhabu ambavyo tayari vina shughulikiwa na sheria zilizopo. Kilicho watisha walio wengi ni kuwagawa watanzania kwani muswada ulikuwa unatazama hisia za Kiislamu kama ushahidi tosha wa makosa ya ugaidi kwa mtu, taasisi au jamii fulani. Na mwisho wa yote ilibainishwa jinsi sheria hiyo itakavyo pingana na Katiba ya nchi na vilevile kujenga fursa kwa mataifa makubwa kuingilia mambo ya ndani na kuvifanya vyombo vya usalama kuwajibika katika kulinda usalama wa mataifa hayo dhidi ya mahasimu wao. Pamoja na yote hayo,hatmae Desemba 14, 2002, Rais aliekuwepo madarakani alisaini muswada huo na kuwa sheria ya nchi. Toka kupitishwa kwa sheria hiyo Waislamu hapa nchini wamekuwa wakihujumiwa na kupata madhara makubwa.

RAIA NA PROPAGANDA ZA AL-SHABAB Tayari serikali ya Tanzania imeanza kuwakamata Waislamu kwa tuhuma za kujihusisha na Al-Shabab. Kabla ya hapo imekuwa ikizuwia shughuli mbalimbali za Kiislamu kwa tuhuma hizo. Watanzania wenye asili ya kisomali wanapekuli na kudhalilishwa na vyombo vya dola sehemu mbalimbali nchini. Serikali pia imekuwa ikizuia shughuli za vyama vya kijamii kwa madai ya uwezekano wa shughuli hizo kutumiwa na Al-Shabab.

Pamoja na muelekeo tuliouona huko nyuma lakini yaelekea kuna hujuma kubwa iliyoandaliwa nyuma ya pazia hili la ugaidi wa Al-Shabab dhidi ya baadhi ya raia wa Tanzania. Tunatahadharisha serikali isijiingize kabisa katika agenda za kidini za kitaifa au kimataifa. Ichukue tahadhari kubwa kwa mashinikizo na masharti ya mataifa makubwa ikiwemo Marekani.

Imetolewa na:
Sheikh
Ponda Issa Ponda
KATIBU

Nakala:
1. Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisia za Kiislamu (T)
2. Shura ya Maimamu Tanzania
3. Wanazuoni wa Kiislamu (HAY-YATUL-ULAMAA)
4. Jumuiya ya Maimamu Zanzibar
5. Jumuiya ya Uamsho (JUMIKI) Zanzibar
6. Wanataaluma wa Kiislamu (TAMPRO)
7. Idara ya Usalama wa Taifa
8. Mabalozi
9. Vyombo vya Habari


Source: http://www.wavuti.com/4/post/2011/11/kamati-ya-kutetea-waislamu-tanzania-yaihadharisha-serikali-kuhusu-wito-wake-dhidi-ya-al-shaabab.html#ixzz1ngLWIQiR

Biblia Inathibitisha Uislamu


Imefasiriwa Na: Abu Bakr Khatib Al-Atrush Wilmen

Mara nyingi watu kuguswa kwa vitendo mbalimbali ambavyo vinafanywa na sisi Waislamu na pia vilivyotajwa katika Biblia. Matendo na Ujumbe huyo yatakuwa katika maeneo kadhaa katika Biblia, Taurat na Injiyl. Sisi tu pamoja katika ’Ibaadah na matendo ambayo yalikuwa yakifanywa na Manabii waliotangulia na Mitume. Na bila shaka dalili hizi ndo zinazidi kututhibitishia kuwa Uislamu ni dini ya hakki kutoka kwa  Allaah na ni dini ya Mitume na Manabii  wote waliotangulia. Kama ituakikishiavyo Qur-aan yenyewe kuwa:

“Semeni nyinyi: Tumemuamini Mwenyezi Mungu na yaletuliyo teremshiwa sisi, na yaliyo teremshwa kwa Ibrahim na Ismail na Is-haaq na Yaaquub na wajukuu zake, na waliyopewa Muusa na ’Iysa, na pia waliyo pewa Manabii wengine kutoka kwa Mola wao Mlezi; hatutafautishi baina ya yeyote katika hao, na sisi tumesilimu kwake.”  Qur-aan 2:136


Hizi zifuatazo ni baadhi ya ’Ibaadah iliyokuwa ikifanywa na Mtume ‘Iysa  (‘Alayhis Salaam):
  
Waislamu Kufanya Harakati Fulani Katika Maombi. Harakati Za Maombi Mbalimbali Katika Biblia

Kutoka kwa Yesu: “Basi, akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akasali:” (Biblia, Mathayo 26:39)

Kutoka kwa Musa: “Kisha Musa akainama mbio kuelekea chini na kusali” (Kutoka 34:8 Biblia)
Kutoka kwa Musa na Haruni: “Musa na Haruni wakaenda kutoka katika Kanisa mbele ya mlango wa hema na wakapiga nyuso zao chini” (Biblia, kitabu cha Hesabu 20:06)

Kutoka kwa Ibrahimu: “Kisha Ibrahimu akaanguka chini kwenye uso wake ...” (Biblia, Mwanzo 17:03)

Kutoka kwa Yoshua: “Kisha Yoshua akaanguka chini kwenye ardhi juu ya uso wake na akainama ...” (Yoshua 5:14 Biblia)

Kutoka kwa Ezra na watu wake: “Na wakapiga magoti wakamwabudu Bwana kwa uso kwenye ardhi “ (Nehemia 8:06 Biblia)
“Popote mnapokutana kufanya ibada nataka wanaume wasali, watu waliojitolea kweli na ambao wanaweza kuinua mikono yao wakisali bila hasira wala ubishi” (Biblia 1 Timotheo 2:08)

“Eliya akainama chini ya ardhi na akainamisha uso wake kati ya magoti yake” (Ya kwanza Wafalme 18:42 Biblia)

“Na Bwana akasema na Musa, akamwambia:” Nenda mbali na mkutano huu, nami baada ya muda nitawaangamiza “. Kisha wakapiga magoti juu ya nyuso zao. “(Biblia ya nne Musa 16:44-45)


Waislamu Husalimiana  Kwa Kusema “Assalamu ’Alaykum”, Maana Yake: “Amani Iwe Nanyi” – Yesu Alikuwa Akisalimiana Kwa Njia Hiyo Hiyo

“Wanafunzi wote wawili walipokuwa wakiwaambia hayo, Yesu mwenyewe akasimama kati yao, akawaambia “Amani iwe juu yenu.! “(Biblia, Luka 24:36)

“Mnapoingia nyumbani wasalimuni wenyeji wake kwa salamu ya amani” (Biblia Mathayo 10:12)


Waislamu Mara Nyingi Hutumia Neno - “Inshaa- Allaah” Ambalo Maana Yake Ni - “Mungu Akipenda” - Maneno Haya Pia Tunapata Katika Biblia

“Ninyi hamjui hata maisha yenu yatakavyokuwa kesho! Ninyi ni kama ukungu unaotokea kwa muda mfupi tu na kutoweka tena. Mngalipaswa kusema: “Bwana akitujalia tutaishi na tutafanya hiki au kile” (Yakobo 4:14–15 Biblia)


Kuomba Kutoka Asubuhi Mpaka Jioni - Waislamu, Kuswali Mara Tano Kwa Siku, Katika Biblia Tunasoma:

“Kuanzia pale jua linapopambazuka mpaka pale linapozama jina la Bwana litukuzwe” (Zaburi 113:3 Biblia)


Kuomba Kwa Nyakati Fulani Kwa Siku - Waislamu Huomba Kwa Nyakati Fulani

“Siku moja, saa tisa alasiri, Petro na Yohane walikuwa wanakwenda Hekaluni, wakati wa sala” (Matendo 03:01)

“Mwanamke mjane kweli, asiye na mtu wa kumsaidia, amemwekea Mungu tumaini lake na huendelea kusali na kumwomba msaada usiku na mchana.(Timotheo 5:05)
“Je, si Mungu basi yake kupata haki ya kuchaguliwa, wakati wao kupiga kelele kwa Mungu mchana na usiku? Je, hao wanapaswa kusubiri?” (Luka 18:07 Biblia)


Waislamu Wanachukua Wudhuu (Kutawadha) Kabla Ya Kuswali. Biblia Inasema Yafuatayo

“Na Musa na Haruni na wanawe baadaye akanawa mikono na miguu kwa maji kutoka humo. Mara nyingi walipokuwa wakenda ndani ya hema ya kukutania, au kuja mbele ya madhabahu, Walikuwa wakijiosha, kama Bwana alivyomwagiza Musa. (Kutoka 40:31-32 Biblia)

“Wale ambao hujitolea na kujisafisha kwa maombi katika bustani, wakiongozwa na mtu ambaye anasimama pale katikati ...” (Isaya 66:17 Biblia)


Biblia Inataja Nyumba Ya Maombi, Hii Inakuwa Tafsiri Ndani Ya Kiarabu Na Kiswahili Masjid Ni Msikiti

“Na akawaambia: Imeandikwa: Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala ... '(Mathayo 21:13 Biblia)
“... Kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa watu wote”. (Isaya 56:7 Biblia)

“Na akawaambia:” Imeandikwa: Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala. Lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang `anyi”. (Biblia St Mathayo 21:13)


Waislamu Kufunga Mwezi Wa Ramadhaan Na Kuwatia Moyo Kufunga Kwa Hiari. Swawmu Imeandikwa Hata  Katika Biblia

“Akafunga siku arubaini mchana na usiku, naye hatimaye kuwa na njaa” (Mathayo 4:02 Biblia)

“Heri wenye njaa na kiu ya kufanya atakavyo Mungu, maana watashibishwa” (Mathayo 5:06 Biblia)

“Mnapofunga, msiwe na huzuni kama wanafiki. Wao hukunja nyuso zao wapate kuonekana na watu kuwa wanafunga... ..” (Mathayo 6:16-18 Biblia)

Sehemu ya Luka ya Biblia unaweza kusoma kama ifuatavyo: “Mtu anaweza pia kufunga kwa hiari katika nyakati za Agano Jipya kwa kawaida juu ya Jumatatu na Alhamisi. Kwa kufanya hivyo kila wiki ilikuwa ni ishara ya maalumu ya uchamungu. (Biblia, Luka 18:12)


Waislamu Kutoa Kwa Maskini (Swadaqah)-Upendo. Katika Biblia Tunasoma

“Jihadharini msije mkafanya matendo yenu mema mbele ya watu kusudi mwonekane nao. La sivyo, Baba yenu aliye mbinguni hatawapeni tuzo. Basi, unapotoa sadaka, usijitangaze. Usifanye kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani ili watu wawasifu. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata malipo yao. Lakini wewe unapotoa sadaka, mkono wako wa kushoto usijue mkono wa kulia umefanya nini. Toa sadaka yako kwa siri. Naye Baba yako aonaye yaliyofichika, atawapa thawabu. “(Mathayo 6:1-4 Biblia)


Waislamu Hawali Nguruwe, Damu, Au Wanyama Wafu. Biblia Pia Inakataza Hilo

“Nguruwe msimle; ana kwato zilizogawanyika lakini hacheui; kwenu huyo ni najisi. Kwa sababu wanyama hao ni najisi msile nyama yao wala msiguse mizoga ya”(Biblia Walawi 11:7-8)

Baadaye katika aya ya 21 ya sura hiyo tunasoma yafuatayo: “usile kitu kilichokufa chenyewe.

“... Na wale wenye kula nguruwe na uchafu mwingine, ndiyo, pia panya, watapotea wote, asema Bwana”. (Isaya 66:17 Biblia)

“Bali tuwapelekee barua kuwaambia wasile vyakula vilivyotiwa najisi kwa kutambikiwa sanamu za miungu; wajiepushe na uasherati; wasile mnyama yeyote aliyenyongwa, na wasinywe damu.”(Biblia Matendo 15:20)

“Ni lazima tu subiri si kwa kula damu. Kwa sababu damu ni roho na roho usile na nyama. Unapaswa kumwaga kwenye ardhi kama maji “. (Kumbukumbu 12:23-24 Biblia)

“Na kama mtu wa nyumba ya Israeli, au mmoja wa wageni ambao wanaishi kati yao, akinywa damu yoyote, nami nitaweka uso wangu dhidi yake ambae anakunywa damu na kumkatilia kwake mbali na watu wake” (Mambo ya Walawi 17:10 Biblia)

“Na hakuna damu yoyote mtayokunywa, ama kwa ndege au mifugo, bila kujali wapi mlipo. Kila mtu anaekunywa damu yoyote, huyo atakatiliwa mbali na watu wake “. (Walawi 7:26-27 Biblia)


Ni Haramu Kwa Waislamu Kunywa Pombe. Biblia Inatueleza Wazi Yafutayo

“Uasherati na pombe lazima uondoshe akilini” (Hosea 4:11 Biblia)

Je, wamesahau kwamba watu wabaya hawataurithi Utawala wa Mungu? Msidanganyike! Watu wanaoishi maisha ya uasherati, wanaoabudu sanamu, wazinzi, au walawiti. wevi, wachoyo, walevi, wasengenyaji, wanyang'anyi, hao wote hawatashiriki Utawala wa Mungu. (Biblia Kwanza Wakorintho 6:9-10)


Katika Uislamu ni haramu Riba. Biblia pia inakataza Riba

“Unaweza kukopa fedha kwa ajili ya maskini yeyote kati yenu, kati ya watu wangu, hivyo ni lazima si kitendo dhidi yake kama walaji riba. Wala kuongeza juu yake faida yoyote” (Biblia, Kutoka 22:25)

“Usichukue faida yoyote ya ndugu yako, ama ya pesa au chakula au kitu kingine chochote ikawa umechukua riba” (Biblia, Kumbukumbu la Torati 23:19)

Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!”. Biblia (Luka 06:34)

“... faida na kuchukua riba - Je, ndo ataishi? Hapana, lazima wafe, lakini kwa sababu yeye kashiriki katika maovu hayo, atakuwa katika adhabu na kifo. damu yake atakuja juu yake “. (Biblia Ezekieli 18:13)

Waislamu huchinja na kutoa Swadaqah ya kondoo mwanamke akijifungua. Hii pia imetajwa katika Biblia.

“Na siku yake ya kujisafisha ikifika, ikiwa ni mvulana au binti,  atachinja kondoo mwenye umri  kwa sadaka ya kuteketezwa ... (Mambo ya Walawi 00:06 Biblia)


Waislamu Hutahiriwa. Yesu Na Ibraahiym Na Manabii Wote Wa Israeli Walikuwa Wakitahiriwa?

Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina Yesu, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla hajachukuliwa mimba '(Biblia, Luka 2:21)

“Na Mungu akamwambia Abrahamu:”Utunze agano langu, wewe na uzao wako baada yako, na vizazi vyote. Na hili ndilo agano kati ya mimi na wewe na uzao wako baada yenu, ambaye mtazishika kila uume kati yenu kutahiriwa katika govi zenu, na hii itakuwa ni ishara ya agano kati ya mimi na wewe. Vizazi, kila mtoto wa kiume kati yenu atatahiriwa, wakati ni umri wa siku nane, kama walivyofanya mtumishi wa kuzaliwa katika nyumba yako na yeye ambaye kanunuliwa kwa fedha za kigeni kutoka kwa watu ambao si wa ukoo wako. Utahiriwa ni kwa mtumishi wenu na aliozaliwa katika nyumba yako na yule uliemnunua kwa fedha. Na ndiyo ahadi yangu katika mwili wako wazi kuwa agano la milele. Lakini mmoja wa watoto wa mataifa mengine mtu mmoja ambaye govi haijawahi kutahiriwa, naye atatengwa na watu wake. Yeye kavunjwa ahadi yangu. (Biblia, Mwanzo 9-14)
“Na Ibrahimu alichukua mtoto wake Ismail na watumishi wake wote, mzaliwa wa nyumba yake na watu waliokuwa wamenunuliwa kwa fedha, kila uume kati ya watu wa Ibrahimu, na kutahiriwa siku hiyo govi yao ambayo Mungu alimwambia. Na Abrahimu alikuwa na miaka tisini na tisa. Wakati govi yake ilitahiriwa na mtoto wake Ismail alikuwa na umri wa miaka kumi na tatu wakati govi yake ilitahiriwa. Tarehe ya siku hiyo Ibrahimu katahiriwa, na mtoto wake Ismail. Na ya watu wote katika nyumba yake, mzaliwa wa watumishi wake wa nyumbani na wale ambao walikuwa wamenunuliwa kwa fedha kutoka mataifa ya nje, walikuwa wametahiriwa pamoja naye “. (Mwanzo 17:23-27 Biblia)

“Na Ibrahimu katahiriwa mtoto wake Isaka alipokuwa na umri wa siku nane, kama Mungu alivyomwamuru”. (Biblia, Mwanzo 21:04)

Kuhusu kutahiri ipo katika biblia: “Agano la Kale liliteuliwa na Mungu kama ishara ya pekee kwa watu wa Israeli, na kama ukumbusho wa ahadi zao pamoja naye. (Kutoka 17:09 a, 3 Mwanzo 0:03, Yohana 7:22) Pamoja na kwamba  mistari yote ya Wayahudi inashuhudia hivyo ikawa ni “moto” na utata suala ambalo lilisaidia kugawa watu baada ya kipindi cha Yesu.


Kuoa Wake Wengi Katika Uislamu. Hata Katika Biblia Kumetajwa Kuoa Wake Wengi

“Akichukua mke mwingine, basi asifanya upungufu wowote katika mlo wa zamani, mavazi au sheria za ndoa”. (Biblia, Kutoka 21:10)

“Kama mtu ana wake wawili, mmoja anayempenda na mwingine ambaye hamuoni ...” (Biblia, Kumbukumbu la Torati 21:15)

“Yeye alikuwa na wake wawili ...” (Biblia, Samuel 01:02)

“Kwa hiyo, Daudi alifika huko pamoja na wake zake wawili ...” (Biblia ya Samuel 02:02)

“Lakini wakati wa usiku aliamka na kuchukua wake wake wawili na watu wake wawili wahuduma na wanawe kumi na mmoja….” (Biblia, Mwanzo 32:22


Uislamu Unaamuru Wanaume Kufuga Ndevu: Tuangalie Biblia Inatwambiaje Kuhusu Suala Hili

“Msikate pande yote ya nywele zenu ya vichwa, wala msikate pande ya ndevu zenu. (Biblia, Walawi 19:27)

Katika Biblia imetajwa katika maeneo mengi, kwamba manabii na waumini walikuwa na ndevu. Tazama kwa mfano Ezra 9:03, Mambo ya Walawi 21:05, Nehemia 13:26
Twitter Bird Gadget