Friday, April 20, 2012

I don't hate Muslims, I hate Islam

'I don't hate Muslims. I hate Islam,' says Holland's rising political star

Geert Wilders, the popular MP whose film on Islam has fuelled the debate on race in Holland, wants an end to mosque building and Muslim immigration. Ian Traynor met him in The Hague

Ian Traynor


Geert Wilders, the right-wing Dutch politician. Photograph: Jerry Lampen/Reuters

A TV addict with bleached hair who adores Maggie Thatcher and prefers kebabs to hamburgers, Geert Wilders has got nothing against Muslims. He just hates Islam. Or so he says. 'Islam is not a religion, it's an ideology,' says Wilders, a lanky Roman Catholic right-winger, 'the ideology of a retarded culture.'

The Dutch politician, who sees himself as heir to a recent string of assassinated or hounded mavericks who have turned Holland upside down, has been doing a crash course in Koranic study. Likening the Islamic sacred text to Hitler's Mein Kampf, he wants the 'fascist Koran' outlawed in Holland, the constitution rewritten to make that possible, all immigration from Muslim countries halted, Muslim immigrants paid to leave and all Muslim 'criminals' stripped of Dutch citizenship and deported 'back where they came from'. But he has nothing against Muslims. 'I have a problem with Islamic tradition, culture, ideology. Not with Muslim people.'

Wilders has been immersing himself in the suras and verse of seventh-century Arabia. The outcome of his scholarship, a short film, has Holland in a panic. He is just putting the finishing touches to the 10-minute film, he says, and talking to four TV channels about screening it.

'It's like a walk through the Koran,' he explains in a sterile conference room in the Dutch parliament in The Hague, security chaps hovering outside. 'My intention is to show the real face of Islam. I see it as a threat. I'm trying to use images to show that what's written in the Koran is giving incentives to people all over the world. On a daily basis Moroccan youths are beating up homosexuals on the streets of Amsterdam.'

Wilders is lucid and shrewd and the provactive soundbites trip easily off his tongue. He was recently voted Holland's most effective politician. If 18 months ago he sat alone in the second chamber or lower house in The Hague, his People's Party now has nine of 150 seats and is running at about 15 per cent in the polls. His Islam-bashing seems to be paying off. And not only in Holland. All across Europe, the new breed of right-wing populists are trying to revive their political fortunes by appealing to anti-Muslim prejudice.

A few months ago the Swiss People's Party of the pugnacious billionaire Christoph Blocher won a general election while simultaneously running a campaign to change the Swiss constitution to ban the building of minarets on mosques. Last month in Antwerp, far-right leaders from 15 European cities and from political parties in Belgium, Germany and Austria got together to launch a charter 'against the Islamisation of western European cities', reiterating the call for a mosque-building moratorium.

'We already have more than 6,000 mosques in Europe, which are not only a place to worship but also a symbol of radicalisation, some financed by extreme groups in Saudi Arabia or Iran,' argued Filip Dewinter, leader of Belgium's Flemish separatist party, the Vlaams Belang, who organised the Antwerp get-together. 'Its minarets are six floors high, higher than the floodlights of the Feyenoord soccer stadium,' he said of a new mosque being built in Rotterdam. 'These kinds of symbols have to stop.'

Where a few years ago the far right in Europe concentrated its fire on immigration, these days Islam is fast becoming the most popular target. It is a campaign that is having mixed results. In Switzerland, the Blocher party has been highly successful. In Holland, Wilders is thriving by constantly poking sticks in the eyes of the politically correct Dutch establishment. But when Susanne Winter ran for a seat on the local council in the Austrian city of Graz last month by branding the Prophet Muhammad a child molester, she lost her far-right Freedom Party votes.

For the mainstream centre-right in Europe, foreigner-bashing is also backfiring. Roland Koch, the German Christian Democrat once tipped as a future Chancellor, wrecked his chances a fortnight ago by forfeiting a 12-point lead in a state election after a campaign that denounced Muslim ritual slaughter practices and called for the deportation of young immigrant criminals.

Wilders echoes some of the arguments against multiculturalism that have convulsed Germany in recent years. Like many on the traditional German right, he wants the European Judaeo-Christian tradition to be formally recognised as the dominating culture, or Leitkultur. 'There is no equality between our culture and the retarded Islamic culture. Look at their views on homosexuality or women,' he says.

But if Wilders shares positions and aims with others on the far right in Europe, he is also a very specific Dutch phenomenon, viewing himself as a libertarian provocateur like the late Pim Fortuyn or Theo van Gogh, railing against 'Islamisation' as a threat to what used to be the easy-going Dutch model of tolerance.

'My allies are not Le Pen or Haider,' he emphasises. 'We'll never join up with the fascists and Mussolinis of Italy. I'm very afraid of being linked with the wrong rightist fascist groups.' Dutch iconoclasm, Scandinavian insistence on free expression, the right to provoke are what drive him, he says.

He shrugs off anxieties that his film will trigger a fresh bout of violence of the kind that left Van Gogh stabbed to death on an Amsterdam street and his estranged colleague Ayaan Hirsi Ali in hiding, or the murderous furore over the Danish cartoons in 2005.

The Dutch government is planning emergency evacuation of its nationals and diplomats from the Middle East should the Wilders film be shown. It is alarmed about the impact on Dutch business. 'Our Prime Minister is a big coward. The government is weak,' says Wilders. 'They hate my guts and I don't like them either.'

And if people are murdered as a result of his film? 'They say that if there's bloodshed it would be the responsibility of this strange politician. It's almost a self-fulfilling prophecy. They're creating an atmosphere. I'm not responsible for using democratic means and acting within the law. I don't want Dutch people or Dutch interests to be hurt.'

But he does want to create a stir. 'Islam is something we can't afford any more in the Netherlands. I want the fascist Koran banned. We need to stop the Islamisation of the Netherlands. That means no more mosques, no more Islamic schools, no more imams... Not all Muslims are terrorists, but almost all terrorists are Muslims.'

Free speech or hate speech? 'I don't create hate. I want to be honest. I don't hate people. I don't hate Muslims. I hate their book and their ideology.'

For more than three years, Wilders has been paying for his 'honesty' by living under permanent police guard as the internet bristles with threats on his life. He has lived in army barracks, in prisons, under guard at home. 'There's no freedom, no privacy. If I said I was not afraid, I would be lying.'

There is little doubt that if Wilders's film exists - and it's shrouded in secrecy - and is broadcast, it will be construed as blasphemy in large parts of the world and may spark a new bloody crisis in relations between the West and the Muslim world.

He does not seem to care. 'People ask why don't you moderate your voice and not make this movie. If I do that and not say what I think, then the extremists who threaten me would win.'

Source: Guardian

Adabu za kustanji (Kuchamba)


Kustanji/Kuchamba ni kusafisha na kuondoa najisi iliyotoka katika mojawapo ya tupu {uchi}mbili au zote mbili; tupu ya mbele na ya nyuma kwa kutumia maji twahara au kinachosimama memo/mahala pa maji wakati wa kukosekana maji kama vile mawe, karatasi, kitambaa, majani na kadhalika. Mchambaji ahakikishe amejisafisha vema kiasi cha kutobakia athari ya najisi iliyotoka; ikiwa ni mkojo au mavi.
Kustanji/Kuchamba baada ya kukidhi haja ni WAJIBU/FARADHI kama tutakavyoona katika kauli za Mtume – Rehma na Amani zimshukie – katika maelezo yajayo.

VITU VITUMIKAVYO KATIKA KUSTANJI
Inajuzu/inafaa kustanji (kuchamba) kwa kutumia maji mutlaq (maji halisi) ambayo ndiyo asili katika kujitwahirisha na najisi. Pia inajuzu kustanji kwa kila kitu chenye sifa zifuatazo :
  1. Kigumu (kigogofu)
  2. Chenye Kuparuza (kisichoteleza)
  3. Kinachoweza kuondosha najisi.
Vitu vyenye sifa hizi ni kama mawe, karatasi, kitambaa na kadhalika. Ni vema kustanji, mtu akaanza kwa kutumia mawe/karatasi kisha ndio akamalizia na maji. Kufanya hivyo ni kwa sababu mawe/karatasi huondosha juta (dhati) ya najisi na maji huondosha athari ya najisi bila ya kuchangayika na juta lake. Ikiwa atatumia kimojawapo baina ya mawe/karatasi na maji, basi ni bora akatumia maji kwani ndiyo pekee yenye uwezo wa kuondosha juta (dhati) na athari ya najisi, kinyume na mawe na nduguze {karatasi, kitambaa na kadhalika}.
Imepokelewa kutoka kwa Anas Ibn Maalik – Allah amuwie Radhi – amesema : Mtume wa Allah alikuwa akiingia mahala pa kukidhi haja, mimi na kijana wa rika langu tukimbebea chombo cha maji na fimbo/mkuki mfupi, basi akistanji kwa kutumia maji. Bukhariy na Muslim.
Maelezo : Fimbo/Mkuki ulikuwa ukitumika kama sitara na alama wakati wa kuswali ili mtu asiweze kupita mbele.
Imepokewa na Ibn Masoud – Allah amuwie Radhi – amesema : Mtume – Rehma na Amani zimshukie – alienda kukidhi haja na akaniamrisha nimletee mawe matatu. Al-Bukhariy.
USISTANJI kwa kutumia najisi nyingine iliyo kavu au kitu kilichonajisika tayari kwani huenda kikaizidisha athari ya najisi badala ya kuipunguza. 
Kadhalika ni haramu kustanji kwa kilicho chakula cha binadamu kama vile mkate au chakula cha majini kama vile mifupa. Amesema Bwana Mtume – Allah amshushie Rehma na Amani – "Msistanji kwa (kutumia) kinyesi cha wanyama wala mifupa kwani hiyo (mifupa) ni chakula cha ndugu zenu majini" Tirmidhiy.
ADABU/TARATIBU ZA KUFUATA KATIKA KUKIDHI HAJA NA KUSTANJI (KUCHAMBA)
Sheria imeweka taratibu ambazo muislamu anapaswa kuzichunga na kuzifuata wakati wa kukidhi haja na kustanji. Taratibu hizi tutazigawa katika mafungu/sehemu zifuatazo :

A. ADABU/TARATIBU ZINAZOFUNGAMANA NA MAHALA PA KUKIDHIA HAJA
Imemlazimu mkidhi haja, ajiepushe kukidhi haja katika :
  1. Njia ya watu au mahala wanapokaa, hii ni kutokana na kero na maudhi yatakayowapata. Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah – Allah amuwie Radhi – kwamba Mtume – Rehma na Amani zimshukie – amesema : "Yaogopeni mambo mawili yaletayo laana" (Maswahaba) wakauliza : Ni yapi mambo mawili hayo ? (Mtume) akajibu : "Ni yule ambaye anajisaidia katika njia ya watu au kivuli chao" Muslim.
  2. Tundu iliyopo ardhini au ufa wa ukuta/kiambaza. Hii ni kwa sababu ya kumlinda na kumuepusha mkidhi haja na madhara yanayoweza kumpata. Kwani anaweza akawamo ndani ya shimo/ufa mdudu mwenye kudhuru kama vile nge au nyoka, huyu akakerwa na haja akaamua kumtokea mtu na kumdhuru. Imepokelewa kutoka kwa Abdillahi ibn Sarjisi, amesema : Amekataza Mtume wa Allah – Rehema na Amani zimshukie – kukojoa katika tundu. Abuu Daawood.
  3. Chini ya mti utoao matunda. Hii ni kwa ajili ya kuyahifadhi na kuyalinda matunda yadondokayo yasipatwe na najisi. Ni mamoja ikiwa matunda hayo yanaliwa au hayaliwi lakini yana manufaa mengine kama dawa.
  4. Maji yaliyotuama (yasiokwenda). Hii ni kutokana na kichefuchefu watumiaji wa maji hayo yakiwa ni mengi yasiyoharibika na najisi na kuyanajisi yakiwa machache na hivyo kuyafanya yasifae kutumika. Imepokelewa kutoka kwa Jabir – Allah amuwie Radhi – kutoka kwa Mtume – Rehema na Amani zimshukie – kwamba (Mtume) amekataza kukojoa katika maji yaliyotuama". Muslim.
Kunya ni aula zaidi kwa kukatazwa

B. ADABU/TARATIBU ZENYE KUFUNGAMANA NA UINGIAJI NA UTOKAJI MAHALA PA KUKIDHI HAJA
Ni Vema kwa mwenye kutaka kukidhi haja, atangulize mguu wake wa kushoto wakati wa kuingia chooni na mguu wa kulia wakati wa kutoka chooni, kama tulivyofundishwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu. Kadhalika asiingie na chochote chenye jina la Mwenyezi Mungu au jina lolote tukufu kama vile jina la Mtume au aya ya Qurani Tukufu. Bali imemlazimu muislamu kukivua kitu hicho wakati wa kuingia chooni. Pia imesuniwa kuleta dua wakati wa kuingia chooni. Pia imesuniwa kuleta dua zilizothibiti kutoka kwa Bwana Mtume kabla na baada ya kutoka chooni.
Aseme kabla ya kuingia chooni :
BISMILLAH ALLAHUMMA INNIY AUDHUBIKA MINAL KHUBUTHI WAL-KHABAITH. Al-Bukhariy na Muslim.
Na aseme baada ya kutoka :
GHUFRAANAKA AL-HAMDU LILLAHIL-LADHIY ADH-HABA ANNIYL-ADHA WA-A’AFANIY. Abu Dawood, Al-tirmidhi, Ibn Majah na Al-twabraniy.

C. ADABU/TARATIBU ZIFUNGAMANAZO NA UPANDE WA KUELEKEA WAKATI WA KUKIDHI HAJA :
Ni haramu kwa mwenye kukidhi haja kuelekea Qiblah au kukipa mgongo. Uharamu huu ni iwapo anakidhi haja mwandani, wala hapana chenye kumsitiri wakati wa kukidhi haja yake. Na imeshurutizwa sitara isiwe mbali nae zaidi ya dhiraa tatu za binadamu sawa na sentimeta 150 takriban. Ikiwa jengo analotumia limeandaliwa maalum kwa ajili ya kukidhia haja (chooni), basi si haramu, bali inajuzu kuelekea na kulipa mgongo Qiblah kwa kuwa pana sitara.
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Ayyuub Al-Answariy – Allah amuwie Radhi – kutoka kwa Mtume –Rehma na Amani zimshukie – amesema "mnapokwenda chooni msielekee Qiblah wala msikipe mgongo kwa (kukidhi) haja ndogo au kubwa, lakini elekeeni mashariki na magharibi". Al-Bukhariy na Muslim.

D. ADABU/TARATIBU ZINAZOFUNGAMANA NA HALI YA KUKIDHI HAJA :
Ni vema kwa mwenye kukidhi haja akategemea mguu wake wa kushoto na kuusimamisha/kuunyoosha mguu wa kulia, hivi ndivyo anavyotakiwa akae wakati wa kukidhi haja. Hekima ya ukaaji huu ni kuifanya haja itokee kwa wepesi kama vile unavyomimina kilichomo ndani ya chupa kwa kuinamisha upande upande. Kadhalika anatakiwa wakati wa kukidhi haja asiangalie juu, utupu wake wala kile kimtokacho. Pia ni karaha kuzungumza wakati anakidhi haja.
Imepokelewa na Ibn Umar –Allah amuwie Radhi – kwamba mtu mmoja alipita ilhali Mtume wa Mwenyezi Mungu – Rehma na Amani zimshukie – akikidhi haja ndogo, (mtu yule) akamtolea salamu, (Mtume) hakumjibu. Muslim.
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Said – Allah amuwie Radhi – amesema ; Nimemsikia Mtume – Rehma na Amani zimshukie – akisema : "Wasitoke watu wawili wakaenda kukidhi haja, hali ya kufunua tupu zao huku wakizungumza, hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu hulichukia hilo" Abu Dawood na wengineo.
Maelezo : Inakisiwa/Inapimiwa juu ya maneno (mazungumzo) mambo mengine kama vile kula, kunywa na kuchezeachezea utupu (uchi).

Kustanji/kuchamba kwa kutumia mkono wa kushoto : Anatakiwa mwenye kukidhi haja atumie mkono wake wa kushoto kusafisha mahala ilipotokea najisi kwani ni karaha kutumia mkono wa kulia.
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Qatadah – Allah amuwie Radhi – kutoka kwa Mtume – Rehema na Amani zimshukie – amesema : "Anapokojoa mmoja wenu, basi asiishike dhakari yake kwa mkono wa kulia na wala asistanji/asichambe kwa mkono wa kulia".
Kadhalika miongoni mwa adabu, anatakiwa mwenye kukidhi haja mawandani; nje ya jengo lililoandaliwa kwa kukidhia haja (chooni), atafute mahala pa faragha palipo mbali na watu. Watu wasimuone wala kusikia harufu ya choo chake au sauti ya mashuzi yake. Imepokelewa kwamba Mtume – Rehema na Amani zimshukie – alikuwa anapotaka kwenda kujisaidia huenda mbali mpaka mtu asiweze kumuona. Abu Dawood na Al-Tirmidhiy.

Vile vile anatakiwa asiisege/asiipandishe nguo yake ikiwa ni shuka/msuli mpaka akurubiapo ardhi, sio anaanza kuvua nje kabla hajaingia ndani. Afanye hivyo kwa ajili ya kuusitiri utupu wake, jambo ambalo limeamrishwa na sheria.

Kisa cha Msikiti wenye jina la ajabu kupita yote Ulimwenguni

Kifuatacho ni kisa kilichoandikwa ndani ya kitabu kiitwacho 'Maajabu katika historia ya utawala wa Al Othmania (Ottoman empire)'.

Mwandishi wa kitabu hicho Ustadh Arukhan Muhammad Ali ameandika yafuatayo;

"Yupo kati yenu aliyewahi kusikia juu ya msikiti wenye jina la ajabu kama hili? Jina la msikti ni (Nishakula mimi).

Basi hili ni jina la msikiti uliopo katika eneo la Fateh katika mji wa Istanbul, na jina lake kwa lugha ya Kiturki ni 'Sanikiy Yadam', na maana yake (Nishakula mimi!), na sababu ya kupewa jina hili la ajabu ni kisa kizuri cha ajabu chenye ibra ndani yake kwa mwenye kuzingatia."

Anaendelea kusema Ustadh Arukhan;

"Katika kijiji hiki alikuwa akiishi mcha Mungu mmoja fakiri jina lake Khayruddin Kajji Afandi. Na sahibu yetu huyu alikuwa kila anapokwenda sokoni akatamani kununua tunda au nyama au haluwa, alikuwa akisema nafsini mwake; "Sanikiy Yadam', (Nishakula mimi!), kisha hanunui tena tunda lile au nyama ile au haluwa ile na badala yake hurudi nyumbani na kuziingiza pesa zenye thamani ya kununulia vitu hivyo ndani ya kisanduku chake na kuzidunduliza kidogo kidogo.

Na baada ya miaka mingi kupita huku akijinyima vyakula vya anasa visivyo vya lazima na kula vyakula vya dharura tu, pesa zile zikaongezeka akaweza kupata thamani ya kujenga msikiti mdogo kijijini pake.

Na kwa vile watu wa kijiji chake wanakijua kisa chake mcha Mungu huyu fakiri na namna alivyoweza kuujenga, wakaupa msikiti wake huo jina la; "Sanikiy Yadam', na maana yake; (Nishakula mimi!)."


Ibra tunayopata katika kisa hiki;

Kiasi gani cha pesa tungeweza kukusanya kwa ajili ya masikini na wenye kuhitaji misaada, na qasri ngapi tugeweza kujijengea huko Peponi Inshaallah, lau kama kila mmoja wetu baada ya kwisha kula, ataweza kujinyima kununua kile kisicho cha dharura, ambavyo ni vingi mno na kutenga thamani ya vitu hivyo kwa ajili ya kuwasaidia ndugu zake?

Ndugu yangu Muislamu! Mtume wetu mtukufu (SAW) alikuwa mkarimu sana, na katika mwezi huu mtukufu alikuwa mkarimu kupita kiasi. Imepokelewa katika hadithi sahihi kuwa; 'Alikuwa mkarimu kupita upepo uliopelekwa (kwa ajili ya kueneza rehma na baraka kila mahala)'.

Jaribu kuifanyia kazi hadithi hii kwa kutenga kila siku kiasi kidogo tu cha pesa baada ya kuacha kununua baadhi tu ya vile visivyo vya lazima, tena baada ya kwisha kula, kisha kwa pesa hizo uingize furaha ndani ya nyoyo za ndugu zako wenye dhiki na shida ambao ni wengi sana! Na kwa njia hii utaweza kujijengea qasri nyingi huko Peponi – Inshaallah

Majina 99 ya Mwenyezi Mungu

Mwenyezi Mungu S.W.T. katuamrisha sisi Waislamu katika Kitabu Chake, Qurani Tukufu, tumuombe kwa kutumia majina Yake. Kama alivyosema katika Suratil Israa aya ya 110, “

 قُلْ ادْعُوا اللَّهَ أَوْ ادْعُوا الرَّحْمَانَ أَيًّا مَا تَدْعُوا فَلَهُ الأَسْمَاءُ الْحُسْنَى…

Maana yake, “Sema: “Mwombeni Allah (Mwenyezi Mungu), au mwombeni Rahman (Mwingi wa Rehema), kwa jina lolote mnalo mwita. Kwani Yeye ana majina mazuri mazuri…”

Pia Mwenyezi Mungu S.W.T. kasema katika Suratil A`araaf aya ya 180, “

 وَلِلَّهِ الأَسْمَاءُ الْحُسْنَى فَادْعُوهُ بِهَا وَذَرُوا الَّذِينَ يُلْحِدُونَ فِي أَسْمَائِهِ…

Maana yake, “Na Mwenyezi Mungu ana majina mazuri mazuri; muombeni kwayo. Na waache wale wanaoharibu utakatifu wa majina Yake…”
Na Mtume S.A.W. kasema katika Hadithi ilyopokelewa na Abu Huraira R.A.A. na iliyotolewa na Ahmad, “

‘‘إِنَّ لِلَّهِ تِسْعَةً وَتِسْعِينَ اسْمًا ، مِائَةً إِلاَّ وَاحِدًا مَنْ أَحْصَاهَا دَخَلَ الْجَنَّةَ’’

Maana yake, “Hakika Mwenyezi Mungu ana majina tisini na tisa. Majina mia isipokuwa moja. Atakayeyahifadhi (majina haya na kujua maana yake) ataingia Peponi.”

Pia Mtume S.A.W. kasema katika Hadithi ilyopokelewa na Abu Huraira R.A.A. na iliyotolewa na L-Bukhari, “

‘‘لِلَّهِ تِسْعَةٌ وَتِسْعُونَ اسْمًا ، مِائَةٌ إِلاَّ وَاحِدًا ، لا يَحْفَظُهَا أَحَدٌ إِلاَّ دَخَلَ الْجَنَّةَ’’

Maana yake, “Mwenyezi Mungu ana majina tisini na tisa. Majina mia isipokuwa moja. Hakuna atakayeyahifadhi (majina hayo na kujua maana yake) isipokuwa ataingia Peponi.”

Ingawa Mwenyezi Mungu Mtukufu katuelezea kwamba majina Yake ni tisini na tisa, lakini hata hivyo majina Yake ni zaidi kuliko hivyo. Hakuna mtu yeyote yule hapa duniani anayeyajua majina Yake yote isipokuwa Mwenyewe Muumba wa mbingu na ardhi. Na Majina haya tisini na tisa yanatafsiri sifa Zake nzuri ambazo sifa hizo hazilingani na sifa za viumbe Wake. Ndio maana Mwenyezi Mungu S.W.T. katuamrisha wakati tunapotaka kumuomba basi kwanza kabla ya kuomba dua tumuombe kwa majina hayo, halafu tuombe tunachotaka kuomba. Na wakati wa kumuomba tuwe katika tohara na moyo na kiwiliwili vimnyenyekee Mola Mtukufu, wala tusijishughulishe na mambo mengine.

Ndio maana Mtume S.A.W. kasema,

“Mwenyezi Mungu hapokei dua ya mtu yule moyo wake umeghafilika wakati anapoomba.” 

Na majina hayo tisini na tisa yametajwa na Mtume S.A.W. kama yalivyokuja katika Hadithi iliyopokelewa na Abu Huraira R.A.A. na kutolewa na Ttirmidhi.

Na anayetaka kuomba dua kwanza asome,

“AUDHU BILLAAHI MINA SHAITAANI RRAJIYM. BISMI LLAAHI RRAHMAANI RRAHIYM: ALLAAHUMMA INNIY ATAWAJJAHU ILAIKA BIASMAA-IKAL HUSNAA YAA MAN HUWA, “

‘‘اللَّهُ الَّذِي لا إِلَهَ إِلاَّ هُوَ ، الرَّحْمَنُ ، الرَّحِيمُ ، الْمَلِكُ ، الْقُدُّوسُ ، السَّلامُ الْمُؤْمِنُ ، الْمُهَيْمِنُ ، الْعَزِيزُ ، الْجَبَّارُ ، الْمُتَكَبِّرُ ، الْخَالِقُ ، الْبَارِئُ ، الْمُصَوِّرُ ، الْغَفَّارُ ، الْقَهَّارُ ، الْوَهَّابُ ، الرَّزَّاقُ ، الْفَتَّاحُ ، الْعَلِيمُ ، الْقَابِضُ ، الْبَاسِطُ ، الْخَافِضُ ، الرَّافِعُ ، الْمُعِزُّ ، الْمُذِلُّ ، السَّمِيعُ ، الْبَصِيرُ ، الْحَكَمُ ، الْعَدْلُ ، اللَّطِيفُ ، الْخَبِيرُ ، الْحَلِيمُ ، الْعَظِيمُ ، الْغَفُورُ ، الشَّكُورُ ، الْعَلِيُّ ، الْكَبِيرُ ، الْحَفِيظُ ، الْمُقِيتُ ، الْحَسِيبُ ، الْجَلِيلُ ، الْكَرِيمُ ، الرَّقِيبُ ، الْمُجِيبُ ، الْوَاسِعُ الْحَكِيمُ ، الْوَدُودُ ، الْمَجِيدُ ، الْبَاعِثُ ، الشَّهِيدُ ، الْحَقُّ ، الْوَكِيلُ ، الْقَوِيُّ ، الْمَتِينُ ، الْوَلِيُّ ، الْحَمِيدُ ، الْمُحْصِي ، الْمُبْدِئُ ، الْمُعِيدُ ، الْمُحْيِي ، الْمُمِيتُ ، الْحَيُّ ، الْقَيُّومُ ، الْوَاجِدُ ، الْمَاجِدُ ، الْوَاحِدُ ، الصَّمَدُ ، الْقَادِرُ ، الْمُقْتَدِرُ ، الْمُقَدِّمُ ، الْمُؤَخِّرُ ، الأَوَّلُ ، الآخِرُ ، الظَّاهِرُ ، الْبَاطِنُ ، الْوَالِيَ ، الْمُتَعَالِي ، الْبَرُّ ، التَّوَّابُ ، الْمُنْتَقِمُ ، الْعَفُوُّ ، الرَّءُوفُ ، مَالِكُ الْمُلْكِ ذُو الْجَلالِ وَالإِكْرَامِ ، الْمُقْسِطُ ، الْجَامِعُ ، الْغَنِيُّ ، الْمُغْنِي ، الْمَانِعُ ، الضَّارُّ ، النَّافِعُ ، النُّورُ ، الْهَادِي ، الْبَدِيعُ ، الْبَاقِي ، الْوَارِثُ ، الرَّشِيدُ ، الصَّبُوْرُ’’

ALLAAHU LLADHIY LAA ILAAHA ILLA HUWA (Yeye Ndiye Mwenyezi Mungu Ambaye hapana mungu isipokuwa Yeye tu), ARRAHMAANU (Mwingi wa rehema), ARRAHIYMU (Mwenye kurehemu), AL-MALIKU (Mfalme wa milele), AL-QUDDUWSU (Mtakatifu, ametakasika na sifa zote chafu), ASSALAAMU (Mwenye kuleta amani), AL-MU-UMINU (Mtoaji wa amani), AL-MUHAYMINU (Mwenye kuyaendesha Mwenyewe mambo Yake), AL-`AZIYZU (Mshindi katika mambo Yake), AL-JABBAARU (Anayefanya analolitaka), AL-MUTAKABBIRU (Mkubwa), AL-KHAALIQU (Muumbaji), AL-BAARI-U (Mtengenezaji), AL-MUSAWWIRU (Mtia sura), AL-GHAFFAARU (Mwenye kusamehe), AL-QAHHAARU (Mwenye nguvu juu ya kila kitu), AL-WAHHAABU (Mpaji mkuu), ARRAZZAAQU (Mwenye kuruzuku), AL-FATTAAHU (Hakimu), AL-`ALIYMU (Mjuzi wa kila kitu), AL-QAABIDHU (Mwenye kunyima au kuzuia), AL-BAASITU (Mwenye kutoa), AL-KHAAFIDHU (Mfedheheshaji waovu), ARRAAFI`U (Mpandisha daraja), AL-MU`IZZU (Mtoa heshima kwa amtakaye), AL-MUDHILLU (Mnyima heshima kwa amtakaye), ASSAMIY`U (Mwenye kusikia), AL-BASIYRU (Mwenye kuona), AL-HAKAMU (Mwenye kuhukumu), AL-`ADLU (Muadilifu), AL-LLATIYFU (Mwenye kujua yaliyofichikana), AL-KHABIYRU (Mwenye kujua yaliyo dhahiri), AL-HALIYMU (Mpole), AL-`ADHIYMU (Aliye Mkuu), AL-GHAFUWRU (Mwingi wa kusamehe), ASHAKUWRU (Mwenye kushukuru), AL-`ALIYYU (Aliye juu), AL-KABIYRU (Aliye mkuu), AL-HAFIYDHU (Mwenye kuhifadhi), AL-MUQIYTU (Mlinzi), AL-HASIYBU (Mwenye kuhesabu), AL-JALIYLU (Wa hali ya juu), AL-KARIYMU (Mkarimu wa hali ya juu), ARRAQIYBU (Mchungaji), AL-MUJIYBU (Mwenye kujibu), AL-WAASI`U (Mwenye wasaa), AL-HAKIYMU (Mwenye hekima), AL-WADUWDU (Mwenye kupenda waja Wake), AL-MAJIYDU (Mwenye utukufu), AL-BAA`ITHU (Mfufuaji), ASHAHIYDU (Mwenye kushuhudia kila kitu), AL-HAQQU (Wa Haki), AL-WAKIYLU (Mtegemewa), AL-QAWIYYU (Mwenye nguvu), AL-MATIYNU (Aliye madhubuti), AL-WALIYYU (Mlinzi na Msaidizi), AL-HAMIYDU (Mwenye kusifika na kila sifa njema), AL-MUHSIYU (Mwenye kuhesabu), AL-MUBDI-U (Mwenye kuanzisha), AL-MU`IYDU (Mwenye kurejeza), AL-MUHYIYU (Mwenye kuhuisha), AL-MUMIYTU (Mwenye kufisha), AL-HAYYU (Mwenye uhai wa milele), AL-QAYYUWMU (Msimamia kila jambo), AL-WAAJIDU (Mtambuzi), AL-MAAJIDU (Wa kuheshimiwa), AL-WAAHIDU (Mmoja tu), ASSAMADU (Mwenye kukusudiwa kwa kuabudiwa), AL-QAADIRU (Mwenye uwezo wa kufanya au kutokufanya), AL-MUQTADIRU (Mwenye uwezo wa pekee juu ya kila kitu), AL-MUQADDIMU (Mwenye kutanguliza), AL-MU-AKHIRU (Mwenye kuakhirisha), AL-AWWALU (Wa Mwanzo), AL-AAKHIRU (Wa Mwisho), ADHAAHIRU (Wa Dhahiri), AL-BAATINU (Wa Siri), AL-WAALIYA (Mpanga mipango ya watu), AL-MUTA`AALI (Mtukufu Aliye juu), AL-BARRU (Mwema), ATTAWWAABU (Mwenye kupokea toba za waja Wake), AL-MUNTAQIMU (Mlipa kisasi kwa waovu), AL-`AFUWWU (Mwenye kusamehe madhambi), ARRAUFU (Mwenye huruma), MAALIKU L-MULKI DHUL JALAALI WAL IKRAAMI (Mfalme wa wafalme Mwenye utukufu na heshima), AL-MUQSITU (Mtoaji haki sawa kwa kila anayestahiki), AL-JAAMI`U (Mkusanyaji viumbe siku ya Mwisho), AL-GHANIYYU (Tajiri), AL-MUGHNIYU (Mwenye kutajirisha), AL-MAANI`U (Mwenye kuzuia viumbe visidhurike), ADHAARRU (Mwenye kudhurisha), ANNAAFI`U (Mwenye kuleta nafuu), ANNUWRU (Mwenye nuru), AL-HAADIY (Mwongozaji wa kheri), AL-BADIY`U (Mzuaji), AL-BAAQIYU (Mwenye kubakia milele), AL-WAARITHU (Mwenye kurithi kila kitu), ARRASHIYDU (Mwenye kuongoa waja kuiendea njia ya kheri), ASSABUWRU (Mwenye kusubiri).”

Ndoa haramu..

Katika zama za ujahilia kabla ya kuja Uislamu ndoa nyingi zilikuwa zikifanyika ambazo hazikufuata sheria alizohukumu Mwenyezi Mungu S.W.T. zifuatwe. Na kwa sababu hizo ndio maana ulipokuja Uislamu Mtume wetu S.A.W. aliwakataza Waislamu wa zama zake. Na zifuatazo hapo chini ni ndoa ambazo Mtume S.A.W. kazikataza kabisa kwa sababu ni kinyume na sheria ya Kiislamu nazo ni:-

1. NDOA YA MUT`A.
Ndoa ya Mut`a (المتعة) ni ndoa ya haramu na batili iliyokuwa maarufu sana katika zama za ujahilia kabla ya kuja Uislamu. Ulipokuja Uislamu uliruhusu kwenye baadhi ya vita tu kwa dharura. Lakini baada ya hapo ukaharamisha mpaka siku ya Kiyama. Kwani ndoa ya aina hii haina talaka, wala mwanamke kukaa eda na wala kurithiana. Nayo inatokea kwa mapatano kati ya mume na mke kuwa wataoana kisha wataishi kwa muda fulani na kwa kiasi fulani cha mahari baadaye wataachana. Na ndoa ya namna hii inaitwa kwa Kiarabu, “Mut`a,” na kwa Kiswahili, “Kuoa kwa muda mfupi.” Na Mtume S.A.W. aliikataza ndoa ya aina hii na akawapigia marufuku Waislamu wote tokea katika zama za vita vya Kheibar ikiwa ni pamoja na kula nyama ya punda wa kufugwa majumbani. Kama ilivyothibiti katika Hadithi iliyopokelewa na Seyyidna Ali bin Abi Twaalib R.A.A. na waliyokubaliana Wanavyuoni wote, “
‘‘أَنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ نَهَى عَنْ مُتْعَةِ النِّسَاءِ وَعَنْ لُحُومِ الْحُمُرِ الأهْلِيَّةِ زَمَنَ خَيْبَرَ’’
Maana yake, “Hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu S.A.W. amekataza ndoa ya mut`a (muda mfupi) na (kula) nyama ya punda wa (kufugwa) majumbani (tokea) katika zama za vita vya Kheibar.”

2. NDOA YA KUOZANA MADADA AU MABINTI.
Ndoa ya aina hii inatokea wakati mtu anapomshurutishia mtu mwingine kwa kumwambiya, “Niozeshe dada yako nami nikuozesha dada yangu,” au kusema, “Niozeshe binti yako nami nikuozesha binti yangu,” bila ya kutoa mahari nayo ni ndoa ya haramu. Na kwa lugha ya Kiarabu inaitwa, “Shighaar.” Na jambo linalosababisha kubatilisha ndoa ya aina hii ni msemo na msimamo. Kwani inakuwa kama vile kila mmoja wao anasema, “Ndoa yako haifungiki na binti yangu mpaka kwanza mimi nifunge ndoa na binti yako,” ambapo haiwezekani kabisa kwa sababu nani kati yao atakaeanza kufunga ndoa? Na yule atakaeanza kufunga ndoa basi mwingine hapati kuoa! Na ikiwa wameoana mume na mke basi watakuwa wamekwenda kinyume na sheria aliyokuja nayo Mtume wetu S.A.W. kwa hivyo lazima waachanishwe mume na mke. Na ikiwa mume kawahi kumuingilia mkewe basi mke kaharamika na hapo inakuwa lazima watenganishwe wasikutane kabisa. Mtume S.A.W. kaikataza kabisa ndoa ya aina hii ya kushurutishana kuozana madada au mabinti bila ya mahari. Na uthibitisho huu umekuja katika Hadithi iliyopokelewa na Abu Huraira R.A.A. na kutolewa na Muslim, “

‘‘نَهَى رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ عَنِ الشِّغَارِ ، وَالشِّغَارُ أَنْ يَقُولَ الرَّجُلُ لِلرَّجُلِ : زَوِّجْنِي ابْنَتَكَ وَأُزَوِّجُكَ ابْنَتِي ، أَوْ زَوِّجْنِي أُخْتَكَ وَأُزَوِّجُكَ أُخْتِي’’
Maana yake, “Mtume wa Mwenyezi Mungu S.A.W. amekataza ndoa ya mwanamume kumwambiya mwanamume (mwingine): “Niozeshe binti yako nami nikuozeshe binti yangu.” Au “Niozeshe dada yako nami nikuozeshe dada yangu.”

Na pia Hadithi nyingine iliyopokelewa na Ibn `Umar R.A.A. na kutolewa na Muslim, “

‘‘أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ نَهَى عَنِ الشِّغَارِ وَالشِّغَارُ أَنْ يُزَوِّجَ الرَّجُلُ ابْنَتَهُ عَلَى أَنْ يُزَوِّجَهُ ابْنَتَهُ وَلَيْسَ بَيْنَهُمَا صَدَاقٌ’’
Maana yake, “Hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu S.A.W. amekataza ndoa ya mwanamume kumuozesha binti yake ili naye amuozeshe binti yake (au dada yake) na baina yao bila ya mahari.”

3. NDOA YA MWANAMKE ALIEACHWA TALAKA TATU.
Ndoa ya aina hii inatokea wakati mume wa kwanza anayeitwa kwa Kiarabu Muhallal (mwenye kuhalalishiwa) anapopanga kwamba mkewe alieachwa kwa talaka tatu aolewe na mume mwingine anayeitwa kwa Kiarabu Muhallil (mwenye kuhalalisha) kwa muda fulani na kwa mahari fulani kisha mke aachike ili apate kurejea kwa Muhallal. Ndoa ya namna hii ya kupanga kwa mipango ya hila haijuzu katika sheria ya Kiislamu, ila ikiwa mke yule ataolewa na mwanamume mwingine kwa khiari yake na aachike kwa ridhaa yake au mume yule yamfike mauti. Mwenyezi Mungu S.W.T. kasema katika Suratil Baqarah aya ya 230, “

فَإِنْ طَلَّقَهَا فَلا تَحِلُّ لَهُ مِنْ بَعْدُ حَتَّى تَنكِحَ زَوْجًا غَيْرَهُ…
Maana yake, “Na kama amempa talaka (ya tatu) basi (mwanamke huyo) si halali kwake baada ya hapo mpaka aolewe na mume mwingine…” 

Na wote wawili Muhallal na Muhallil wanalaaniwa na Mwenyezi Mungu S.W.T.. Kwa kauli ya Mtume wetu S.A.W. na uthibitisho umekuja katika Hadithi iliyopokelewa na Seyyidna Ali bin Abi Twaalib R.A.A. na kutolewa na Abu Daud, “

‘‘أَنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ : لَعَنَ اللَّهُ الْمُحَلِّلَ وَالْمُحَلَّلَ لَهُ’’
Maana yake, “Mtume wa Mwenyezi Mungu S.A.W. kasema “Mwenyezi Mungu amemlaani anayehalalisha na anayehalalishiwa (katika ndoa za haramu).” 

4. NDOA YA MTU KATIKA IHRAAM.
Ndoa ya aina hii inatokea wakati Mwislamu anapotaka kuoa naye kahirimu kwa ajili ya Hija au Umra. Mtume S.A.W. kasema katika Hadithi iliyopokelewa na Sayyidna `Uthmaan bin `Affaan R.A.A. na iliyotolewa na Muslim,“

‘‘لا يَنْكِحُ الْمُحْرِمُ وَلا يُنْكَحُ وَلا يَخْطُبُ’’
Maana yake, “Haowi aliyehirimu na wala haozeshwi na wala hachumbii.”

5. NDOA KATIKA EDA.
Mwenyezi Mungu S.W.T. amemkataza mwanamume Mwislamu kumuoa mwanamke wa Kiislamu wakati anapokuwa katika eda ya talaka au eda ya kifo cha mumewe kwani ndoa ya namna hizi mbili ni haramu, mwanamke anaruhusiwa kuolewa na mwanamume mwingine wakati kakamilisha eda yake. Kama alivyotuamrisha Mwenyezi Mungu S.W.T., kasema katika Suratil Baqarah aya ya 235, “

…وَلا تَعْزِمُوا عُقْدَةَ النِّكَاحِ حَتَّى يَبْلُغَ الْكِتَابُ أَجَلَهُ…
Maana yake, “…Wala msiazimie kufunga ndoa mpaka muda ulioandikwa (katika eda) ufike mwisho wake...” 

6. NDOA BILA YA WALII.
Kwa sheria ya Kiislamu haimfalii mwanamume Mwislamu kumuoa mwanamke wa Kiislamu bila ya idhini ya walii wake, kwani ndoa ya namna hii ni batili kwa sababu ya kupungua nguzo katika nguzo za ndoa. Kwa kauli ya Mtume S.A.W. katika Hadithi iliyotolewa na L-Bukhari, Muslim, Nnasaai, Ibn Majaah, Haakim na Ibn Habbaan, “

‘‘لا نِكَاحَ إِلا بِوَلِيٍّ’’
Maana yake, “Hapana ndoa ila kwa walii (wake).”

7. NDOA YA MWANAMKE MUSHRIKA.
Mwenyezi Mungu S.W.T. amemharamishia mwanamume Mwislamu kuoa mwanamke Mushrika (anayeabudu masanamu), wala Majusia (anayeabudu moto), wala Saabia (anayeabudu nyota), wala Budhia na wala Burhamia. Na vile vile imeharamishwa kwa mwanamke wa Kiislamu kuolewa na mwanamume Mushrik (anayeabudu masanamu). Kama alivyokataza Mwenyezi Mungu S.W.T., kasema katika Suratil Baqarah aya ya 221, “
وَلا تَنكِحُوا الْمُشْرِكَاتِ حَتَّى يُؤْمِنَّ…
Maana yake, “Wala msiwaoe wanawake washirikina mpaka waamini …” 

Na hekima ya kukatazwa kuwaoa wanawake wa aina hii ni kwa sababu hizi: Mume na mke wanategemewa kuishi wote wawili kwa pamoja na kuwa na mapenzi na huruma. Na makusudio haya hayawezi kuja kwani kila mmoja wao humchukia mwenziwe kwa kule kuwa kila mmoja wao ana ibada tofauti zisizolingana sawa kwa tabia, mila, sheria na desturi. Na ikiwa ndio hivyo, basi maisha ya mume na mke hayawezi kuendelea kwa muda mrefu na wala kuwa imara na mwishowe huvunjika. Na wanawake wenye dini za aina hii kutokana na dini zao haziharamishi kama vile: Khiana, zina, wala haziamrishi mema na wala kukataza mabaya na mengi mengineo. 

Wednesday, April 18, 2012

Quran Reciters Names


Twitter Bird Gadget