Tuesday, April 2, 2013

KIJIJI CHA MISUKULE FEKI CHAFICHULIWA BAGAMOYO



INATISHA na hofu kubwa imetanda katika Kijiji cha Kimange, Wilaya ya Bagamoyo  mkoani Pwani kufuatia baadhi ya viongozi  wa dini kuwatumia vijana wa hapo kama misukule ili wapelekwe kanisani.
Msukule.
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa nia ya viongozi hao wa dini kuteua kijiji hicho na kuwatumia vijana wa hapo kama misukule ni kuwalaghai waumini kwamba wana uwezo wa kufufua watu wanaodaiwa kufa na kuchukuliwa kimazingara.
Gazeti hili limebaini kuwa viongozi hao wa dini wamekuwa wakifanya udanganyifu huo lengo lao likiwa ni kupata waumini wengi katika makanisa yao ambao wamekuwa wakiamini kwamba kweli misukule inarejeshwa katika maisha ya kawaida.
Habari kutoka kijijini hapo zinadai kwamba viongozi wa dini wanaofika katika kijiji hicho wamekuwa wakiwalipa watu wanaojitokeza kuwa misukule bandia kati ya shilingi 200,000  hadi 250,000  kwa kila mtu.
Msukule.
Imegundulika kuwa viongozi hao wa dini  hufanya zoezi hilo kwa siri kubwa na kuna  nyumba ya mchungaji mmoja, nje kidogo ya kijiji hicho ambapo misukule hao feki  hupewa mafunzo ya nini cha kufanya kabla ya kusafirishwa kuelekea Dar es Saalam.
Imeelezwa kuwa misukule husafirishwa kwenye magari yenye vioo vyeusi ‘tinted’ wakiwa wamepakwa matope mwili mzima  na kuvalishwa nguo zilizochanika.
“Wapo wachungaji waliofanya hivyo kwa kuwalaghai waumini wao kwamba wana uwezo wa kufufua watu huku wakijua kwamba lengo lao ni kuwavutia watu wajazane kwenye makanisa yao ili wapate  sadaka nyingi,” kilisema chanzo chetu.

 Uchunguzi  umebaini  kwamba  kuna makanisa  ambayo  yana wafuasi wengi wa kufanya mazingaombwe ya namna hiyo na wamekuwa wakijipatia fedha nyingi ambapo kwa Jumapili moja, hujikusanyia kati ya shilingi 7,000,000 hadi 7,500,000.
Aidha, ‘hukomba’ sadaka wakati wa maombi ya katikati ya wiki kwa kutumia mbinu mbalimbali za kuvuta waumini.
Baadhi ya vijana wa kijiji hicho ambao  waliwahi kurubuniwa na wachungaji baada ya kufuatwa kijijini hapo ni pamoja na Ziada Mlanga (33) na Shakila Ayubu (29).
Katika  mahojiano  na mwandishi wetu kijijini hapo, Ziada alikuwa na haya ya kusema:
“Machi 21, 2011 kaka mmoja (jina tunalihifadhi) anayeishi Kijiji cha Makore jirani na chetu, alinifuata na kunieleza kwamba anahitaji vijana wanne, wa kike  wawili na wa kiume wawili ili wajiunge katika shughuli za sanaa, yaani kuigiza.

“Hata hivyo, alifanikiwa kunipata mimi na Shakila, akatuahidi kutulipa shilingi 350,000 kila mmoja na wazazi wetu kupewa shilingi 100,000 kila mmoja.
“Tulikubali  kufanya hivyo, walituchukua kwa pikipiki hadi Kijiji cha Makore  nyumbani kwa mtu mmoja aliyemtaja kuwa ni mchungaji.

“Tulipofika huko walituweka katika chumba maalum katika nyumba ya huyo mchungaji  ambayo ipo porini, wakatueleza kwamba  tusubiri kuna watu wanakuja kutupa  mafunzo.
“Baada ya muda mfupi walifika watu ambao tulipoongea nao, walitueleza tuvue nguo zote tubaki na za ndani. Tulifanya hivyo, wakatupaka majivu, wakatuvuruga nywele  na kutuvalisha nguo chakavu na ilipofika saa moja usiku, walikuja watu wengine wakiwa kwenye gari yenye vioo vya tinted.
“Walitueleza kwamba tunaelekea jijini Dar es Salaam ambako tukifika tujifanye mazezeta. Tulifika usiku sana na kupelekwa katika kanisa moja (jina linahifadhiwa).

“Ndani ya gari lile kulikuwa na bastola, hatukujua ni ya nini, pale kanisani tulitengenezewa chai. Hata hivyo, tulikataa  kuinywa.
“Baadaye walitueleza kwamba wametufanya vile ili tuonekane kama watu  waliokuwa wamechukuliwa kimazingara na kufanywa misukule na sasa tumeokolewa na mchungaji wa kanisa hilo.
“Kesho yake ilikuwa Jumapili, tuliambiwa tutasimama mbele ya waumini kanisani na tusiseme kitu chochote ili tuje kuanza kuongea kidogo baada ya kuombewa na mchungaji.
 “Hata hivyo, tulipewa majina ya watu mashuhuri waliokufa lakini mimi nilikataa kwa kuwa aliyetajwa kuwa nijifanye ndiyo mimi alikuwa mtu maarufu.
 “Nilijiuliza ndugu zake wangenielewaje? Kitu cha pili ni kwamba nilikataa kwa kuwa fedha tulizokubaliana walikuwa hawajatupatia na tukaona kuwa huo ni udhalilishaji.

“Baada ya kuona tumekataa, walitusihi  tusitoe siri na baadaye tulipewa nguo  nyingine tukavaa na tukapewa shilingi elfu hamsini kila mmoja kama nauli ya kurudia kijijini kwetu Kimange.
“Tulipofika tuliwaeleza wazazi wetu  mambo tuliyofanyiwa wakaona tumedhalilishwa, ikabidi tuje nao Dar es Salaam  tukaenda hadi Kituo cha Polisi  Magomeni na kufungua  kesi.
  “Tuliwaambia polisi kuwa simu na nguo zetu ziko kwa watu hao lakini hadi leo kesi tuliyofungua hatujui ilipofikia na tuliambiwa polisi wamewasiliana na wenzao wa Mkoa wa Pwani.
“Polisi wa Pwani walikuja Dar na kutuchukua hadi Kibaha ambako tulitoa maelezo na tukaenda nao Kijiji cha Makore lakini  hatukumkuta mchungaji huyo, tukaambiwa kuwa alihama baada ya kupata habari kuwa anatafutwa na polisi,” alisema Ziada akiungwa mkono na Shakila.

BABA  WA  ZIADA
Baba wa Ziada aliyejitambulisha kwa jina la Sijali Musini Mlanga, alisema kwamba kitendo walichofanyiwa watoto hao ni cha udhalilishaji na anaiomba serikali kuchukua hatua.
“Hatuwezi kukubaliana na hali hiyo, huo ni utapeli na udhalilishaji mkubwa, hakuna dini  inayoweza kufanya mambo kama hayo, wahusika wachukuliwe hatua,” alisema Mlanga.

MWENYEKITI  WA  KIJIJI  
Mwenyekiti wa Kijiji cha Kimange, Juma Issa  Madinga amekiri kufahamu suala hilo na kukemea kitendo hicho.
“Hao wachungaji hawawezi kuachwa wakifanya mambo hayo na kusababisha kijiji kupakaziwa kuwa ni cha misukule, sasa wananchi wasilaghaiwe na matapeli hao, wakija tena watoe taarifa kwangu,” alisema  mwenyekiti huyo.

Chanzo: Uwazi (Global Publishers)

Sunday, September 23, 2012

When is a terrorist a terrorist?


When is a terrorist a terrorist?
Members of the terrorist Mujahedin-e Khalq Organization (MKO) (file photo)
Members of the terrorist Mujahedin-e Khalq Organization (MKO) (file photo)
Sat Sep 22, 2012 6:2PM GMT
By Danny Schechter
And now, the United States Government through a decision by Secretary of State Hillary Clinton has decided that the Mujahedin-e Khalq, or People’s Mujahedin, that had been on the US State Department’s terrorist list for years, has now been taken off the list."
Related Interviews:
Question: When is a terrorist a terrorist?
Answer: When the US government says so.

When the Mujahedeen in Afghanistan were assassinating members of their government and the Russian troops dispatched to support it they were, in Washington’s view, freedom fighters, even as their enemies branded them terrorists.

When they turned against an Afghan government imposed by the United States or revolted against a US invasion, they were once again branded terrorists.

When armed groups battling Muammar Gaddafi’s government were supported by NATO, they were called freedom fighters. When some recently and allegedly turned violently against the United States which is now dominating Libyan politics, they are once again castigated as terrorists.

And now, the United States Government through a decision by Secretary of State Hillary Clinton has decided that the Mujahedin-e Khalq, or People’s Mujahedin, that had been on the US State Department’s terrorist list for years, has now been taken off the list.

That means they will no longer face financial and legal sanctions.

One day they were feared terrorists, the next day they were not. The “bad guys” became “good guys” with the swipe of a pen.

The New York Times says this feat was accomplished through what it describes as an “extraordinary” lobbying effort costing millions over many years.

“The group, known as the MEK, carried out terrorist attacks in the 1970s and 1980s, first against the government of the Shah of Iran and later against the clerical rulers who overthrew him. Several Americans were among those killed. In the 1980s, it allied with Saddam Hussein, who permitted it to operate from Camp Ashraf.

But by most accounts, the MEK has not carried out violent attacks for many years. While it is described by some critics as cult-like and unpopular with Iranians both inside and outside the country, the group has been able to gather large crowds at rallies in the United States and Europe to press its bid to reverse the United States’ terrorist designation, imposed in 1997,” reports the Times.

The decision comes just before an October 1 cutoff date ordered by a Federal appeals court.

US News explains, “As recently as 2007, a State Department report warned that the MEK, retains "the capacity and will" to attack "Europe, the Middle East, the United States, Canada, and beyond.

The MEK, which calls for an overthrow of the Iranian government and is considered by many Iranians to be a cult, once fought for Saddam Hussein and in the 1970s was responsible for bombings, attempted plane hijackings, and political assassinations. It was listed as a foreign terrorist organization in 1997.

If the State Department does decide to delist MEK, whose name means "People's Holy Warriors of Iran," it will be with the blessing of dozens of congressmen.”

No less than 99 members of Congress-Democrats and Republican alike-signed to a Congressional resolution to take the “holy warriors” off the list.

Just last week at a rally in Paris, none other than former House speaker and hyper conservative Republican presidential candidate Newt Gingrich, now scurrying to pay off his campaign debts, was caught on camera bowing to the French-based movement’s leader Maryam Rajavi.

Top lobbying firms have been paid high fees for rounding up support for MEK

US News explains, “Victoria Toensing of DiGenova and Toensing, a lobbying shop famous for its involvement in the Bill Clinton-Monica Lewinsky scandal, was paid USD110,000 in 2011 to lobby for the resolution. The firm Akin, Gump, Strauss, Hauer and Feld dedicated five lobbyists to getting signatures for the resolution, and was paid USD100,000 in 2012 and USD290,000 in 2011 to do so. Paul Marcone and Association similarly lobbied for the resolution, and received USD5,000 in 2010 and USD5,000 in 2011 for its efforts.”

Glenn Greenwald has reported on Salon, “That close association on the part of numerous Washington officials with a Terrorist organization has led to a formal federal investigation of those officials… paid MEK shill Howard Dean (a former Democratic liberal presidential candidate) actuallycalled on its leader to be recognized as President of Iran while paid MEK shill Rudy Giuliani has continuously hailed the group’s benevolence.”

The ProPublica not for profit media organization has also revealed that a very prominent liberal journalist known for his Watergate reporting was paid to speak up for MEK.

“On a Saturday afternoon last February, journalist Carl Bernstein got up on stage at the grand ballroom of the Waldorf Astoria in Manhattan and delivered a speech questioning the listing of an obscure Iranian group called the Mojahedin-e Khalq (MEK) on the US government list of officially designated foreign terrorist organizations.

The speech, before a crowd an organizer put at 1,500, made Bernstein one of the few journalists who has appeared at events in a years-long campaign by MEK supporters to free the group from the official terrorist label and the legal sanctions that come with it. He told ProPublica that he was paid USD12,000 for the appearance but that, “I was not there as an advocate.”

Bernstein told the crowd that, “I come here as an advocate of the best obtainable version of the truth” and as “someone who believes in basic human rights and their inalienable status.” He also challenged the State Department, saying that if the agency “has evidence that the MEK is a terrorist organization, have a show-cause hearing in court, let them prove it.”

Listening to the talk was a bi-partisan group of prominent politicians including ex-New York City Mayor Rudy Giuliani, former congressman Patrick Kennedy, D-R.I., former Attorney General Michael Mukasey, and former House Speaker Dennis Hastert, R-Ill.

This is a lineup that is hard to rent, much less buy, but MEK and its well connected lobbyists have shown how money makes things happen in Washington.

It shows how porous the terrorism issue too is subject to how changes in political fashions, and how little the media knows or remembers and how open it is to being influenced by insiders, especially when there’s money to be paid for a few hours work.

SOURCE:  http://www.presstv.ir/detail/2012/09/22/263009/when-is-a-terrorist-a-terrorist/ 

Thursday, August 23, 2012

Wasemavyo Wanasayansi


Wasemavyo Wanasayansi

Chaguo langu la Muhammad kuongoza orodha ya watu walioacha athari kubwa dunianilinaweza kuwashangza baadhi ya wasomaji na kuhojiwa na baadhi yao, lakini ndiye mtu pekee katika historia aliyefanikiwa mno kwenye ngazi zote mbili za kisekula na kidini…Yumkini nguvu na athari  husika ya Muhammad kwenye Uislamu ni kubwa mno kuliko atharina nguvu ya Yesu Kristo na Mt. Paulo kwenye Ukristo zikiunganishwa pamoja…

Ni muungano huu usio kifani wa nguvu ya kisekula na kidini ambayo ninahisi inampaMuhammad hadhi ya kuchukuliwa kuwa mtmwenye athari na nguvu kuliko wengine katikahistoria ya binadamu. 

(Michael Hart katika 'The 100, A Ranking of the Most Influential Persons In History,'New York, 1978).
Yafuatayo ni baadhi ya maoni ya wanasayansi juu ya miujiza ya kisayansi katika Qur-aan Tukufu. Maoni yote yamechukuliwa kutoka katika mkanda wa video unaoitwa This is the Truth. Katika mkanda huu wa video, unaweza kuwaona na kuwasikia wanasayansi wakitoa maoni yao yafuatayo. (Tafadhali tembelea www.islam–guide.com/truth kwa ajili ya kupata nakala ya video hiyo, kuiangalia kutoka katika kompyuta mtandaoni au kuangalia video fupi za maoni mtandaoni)


Keith L. Moore

Dr. Moore alikuwa ni Rais wa zamanwa Chama cha Canada cha wana-anatomia, nachamAmerika cha wana-anatomia wa tiba. Alitunukiwa tuzo yenye hadhi kubwaya J.C.B. Grant Award kutokchama cha wana-anatomia wa Canadna mwaka1994 alipokea Tuzo ya mwanachama anayeheshimika (ThHonoured MemberAward) kutoka chama cha wana-anatomia wa Amerika " kwmchangbora katikauwanja wa anatomia ya tiba.

Kwa Maneno yake:
"Kwa kipindi cha miaka mitatu, nimefanya kazi na Kamatiya Embriolojia ya Chuo Kikuu cha MfalmAbdulazimjiniJeddah, Saudi Arabia, nikiwasaidikutafsiri maelezomengi yaliyomo ndani ya Qur'an na Sunnah kuhusu uzaziwa binadamu na maendeleo yakkabla ya kuzaliwa.Mwanzo nilistaajabishwa mno nusahihi na ukweli wamaelezo haya yaliyoandikwa karnya 7 ADkablasayansi ya Embriolojia haijaanzishwa. Ingawa nilikuwanikiifahamu historia tukufu ya wanasayansi wa Kiislamukatika karne ya 10 AD, nbaadhi ya mchango waokwenye tiba na madawa, sikuwnikijua chochote kuhusumambo matukufu yenykushangaza na imani mbalimbali zilizomo ndani ya 
Qur'an naSunnah."


kwenye Kongamano mjini Cairo aliwasilisha mada yushuhuda wa utafiti na kusema:

"Imekuwa furaha kubwa kwangu kutoa mchango katika kufafanua taarifa mbalimbalizilizomo ndanya Qur'an kuhusu maendeleo ya binadamu. Ni wazkwangu kuwa lazimazitakuwa zimemfikia Muhammad kutoka kwMwnyezi Mungu, au Allah, kwa sababusehemu kubwa ymaarifa haya hayakugunduliwa mpaka baada ya karne nyingi kupita. Hii inathibitisha kwamba lazima Muhammad
atakuwa Mtume wa Mungu, au Allah"


Profesa Moore vilevile alieleza kuwa:
"…Kwa kuwa uonyeshaji wa kiinitete cha binadamu nsuala tata, kutokana na mchakato wakuendelea kubadilika wakati wa ukuaji, inapendekezwa kuwa mfummpya wa Uainishajiinaweza kupatikana kwa kutumia masharti yaliyotajwa katika Qur'anna Sunna. Mfumo huounaopendekezwa nrahisi, mpana, unaendana na maarifya kisasa ya Embriolojia.... Utafitimkubwa wa Qur'an na Hadith katika kipindi chmiaka minne iliyopitumeonyesha wazimfumo wa uainishaji wa kiinitete cha binadamu ambao ni wa ajabkutokana na ukwelikwamba uliandikwa tangu karne ya saba AD .. maelezyaliyomo katikQur'an hayawezikuwa yametokana na msingi wa elimu ya sayansi katikkarne ya saba ..."


_____________________

E. Marshall Johnson

Profesa na Mwenyekiti wa Idara ya Anatomia na Maendeleo ya Baolojia, na Mkurugenza wa Taasisi ya Daniel Baugh, Chuo Kikuu cha Thomas Jefferson, Philadelphia, Pennsylvania, Marekani. Ni mwandishi wa zaidi ya machapisho 200. Miongoni mwa kazi zake nyingine aliwahi kuwa Rais wa Chama Teratolojia.

Profesa Johnson alianza kuvutiwa na miujiza ya kisayansi iliyomo ndani ya Qur'an kaika Kongamano la 7 la Tiba lililofanyika Saudi Arabia (1982), baada ya kuundwa kwa kamati maalumu ya kutafiti miujiza ya kisayansi iliyotajwa ndani ya Qur'an na Hadithi. Mwanzo, Profesa Johnson alikataa kukubali kuwa kaika Qur'an na Hadithi kuna maandiko kama hayo. Lakini baada ya majadiliano na Sheikh Zindan alianza kuvutika na hata kuufanya utafiti wake ujikite kwenye maendeleo ya ndani na nje ya kiinitete.

"...kwa ufupi, maelezo ya Qur'an sio tu kwamba yanaelezea juu ya maendeleo muundo wa ndani, bali pia inasisitiza juu ya hatua za ukuaji wa nje, ukuaji wa ndani wa kiinitete, uumbwaji wake na maendeleo yake, ikisisitiza juu ya matukio makubwa yanayotambuliwa na elimu ya sayansi ya kisasa."

"Kama mwanasayansi, ninaweza tu kushughulika na vitu ninavyoweza kuviona kabisa. Ninaweza kuielewa embrolojia na maendeleo ya kibaolojia. Ninaweza kuyaelewa maneno ninayotafsiriwa kutoka ndani ya Qur'an. Kama nilivyotoa mfano hapo awali, kama ningetakiwa kujibadilisha mimi kuwa katika zama hizo, kwa kujua kile ninachofanya leo kuelezea vitu, nisingeweza hata kidogo kuelezea mambo haya yaliyoelezwa…”

_____________________

T.V.N. Persaud

Dr. T. V. N. Persaud ni Profesa wa Anatomia (sayansi inayohusu mwili na viungo vyake jinsi vilivyo, Profesa wa Matibabu ya watoto na magonjwa yao (Pediatrics) na Afya ya Mtoto, na Profesa wa Ukunga, Jinakolojia (Elimuuzazi), na Sayansi ya mambo ya Uzazi katika Chuo Kikuu cha Minatoba, Winnipeg, Manitoba, Kanada. Hapo, alikuwa Mwenyekiti wa Idara ya Anatomia kwa miaka 16. Yeye ni mashuhuri katika uwanja wake. Yeye ni mwandishi au mhariri wa vitabu 22 na amechapisha vitabu zaidi ya tafiti 180 za kisayansi. Mnamo mwaka 1991, alipokea tuzo ya kipekee kabisa iliyotolewa katika uwanja wa Anatomy huko Kanada, J.C.B. Grant Award kutoka katika Chama cha wana-Anatomia wa Kanada. Alipoulizwa juu ya miujiza ya kisayansi katika Qur’an ambayo aliifanyia tafiti, alisema yafuatayo:

Namna nilivyoelezwa ni kwamba, Muhammad alikuwa mtu wa kawaida. Hakuweza kusoma, hakujua (namna ya) kuandika. Kwa kweli, alikuwa asiyejua kusoma. Sisi tunazungumzia kadiri ya miaka elfu moja na mia mbili [kwa kweli kadiri ya miaka elfu moja na mia nne] iliyopita. Unamkuta mtu asiyejua kusoma na kuandika akitoa matamko na kauli zenye maarifa mengi na cha ajabu ziko sahihi kuhusiana na sayansi. Mimi binafsi yangu, sioni ni vipi hii inawezaje kuwa ni bahati nasibu tu. Kuna mambo mengi sana ya uhakika na, kama Dr. Moore, sioni tatizo katika fikra zangu kuwa hii msukumo au uhusiano utokao kwa Mwenyezi Mungu ndio uliomwongoza yeye atoe kauli hizi.”
Profesa Persaud amejumuisha baadhi ya Aayah za Qur’an na Hadiyth za Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika baadhi ya vitabu vyake. Pia aliziwasilisha Aayah na Hadiyth za Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika mikutano kadhaa wa kadhaa.

Sioni ushahidi wowote wa kukanusha fikra ya kwamba mtu huyu Muhammad alikuwa akipata taarifa hizi mahali fulani … hivyo sioni chochote kinachokinzana na fikra ya kuwa Mungu alihusika katika kile alichoweza kukiandika…"
_____________________

Joe Leigh Simpson


Dr. Joe Leigh Simpson ni Mwenyekiti wa Idara ya Ukunga na Jinakolojia (Elimuuzazi), Profesa wa Ukunga na Elimuuzazi, na Profesa wa Vinasaba vya Kimolekuli na Kibinaadamu katika Chuo cha Utabibu cha Baylor, Houston, Texas, Marekani. Hapo kabla alikuwa Profesa wa Ob-Gyn na Mwenyekiti wa Idara ya Ob-Gyn katika Chuo Kikuu cha Tennessee, Memphis, Tennessee, Marekani. Pia alikuwa Rais wa Chama cha Utungishaji Mimba (Fertility Society) cha Marekani. Amepokea tuzo nyingi, ikiwa ni pamoja na Tuzo ya Utambuzi wa Kijamii ya Chama cha ma-Profesa wa Ukunga na Elimuuzazi, mnamo mwaka 1992. Profesa Simpson alizisoma Hadiyth mbili za Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
(Kwa kila mmoja wenu, vijenzi vya kuumbwa kwenu hukusanywa pamoja katika tumbo la uzazi la mama kwa muda wa siku arubaini...)
(Ikiwa siku arubaini na mbili zitapita katika kiinitete, Mwenyezi Mungu Humtuma Malaika ambaye hukitia umbo na kuumba kusikia kwake, kuona, ngozi, minofu na mifupa...)
Alizichunguza Hadiyth mbili hizi za Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwa undani, na kutia maanani kuwa siku arubaini na mbili za kwanza huwa na hatua dhahiri kuzitofautisha za mwanzo wa kiinitete. Yeye binafsi alishawishika na usahihi wa kauli ya Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). kisha, katika mkutano mmojawapo alitoa maoni yafuatayo.
“Kwa hivyo, Hadith hizo mbili zilizotajwa zinatupatia ratiba makhususi kuhusu maendeleo makuu ya kiinitete kabla ya siku arubaini. Kwa mara nyingine, nukta muhimu imeshawekwa, nadhani kwa kurudiwarudiwa na wasemaji wengine asubuhi hii, Hadiyth hizi haziwezekani kuwa zimepatikana kwa kufuata msingi wa ujuzi wa kisayansi uliokuwepo katika zama za kuandikwa kwake... Kinachofuatia, nadhani, kwamba si tu kuwa hakuna ukinzani baina ya jenetiki na Dini , lakini, kwa kweli, Dini huiongoza sayansi kwa kuongeza ufunuo kwa baadhi ya njia za kisayansi za kimapokeo, kwamba kunakuwepo kauli katika Qur’an zilizoonesha baada ya karne nyingi kuwa thabiti, ambazo zinasaidia kuwa elimu iliyomo katika Qur’an imepatikana kutoka kwa Mwenyezi Mungu".
_____________________

Alfred Kroner


Profesa katika idara ya Geosciences, Chuo Kikuu cha Mainz, Ujerumani.
Profesa Kroner ni miongoni mwa wanajiolojia maarufu duniani, akifahamika kwa wanasayansi wenzake kwa ukosoaji wake dhidi ya nadharia mbalimbali za wanasayansi wakubwa katika fani yake. Sheikh cAbdul-Majeed A. Zindani alikutana naye na kumpatia aya na hadithi kadhaa alizozifanyia utafiti na kuzitolea maoni.

"Nikitafakari mahali Muhammad alitoka... Naddhani haiwezekani kuwa alikuwa akijua vitu kama vile asili ya ulimwengu inayokubaliwa na kila mtu, kwa sababu ni miaka ya hivi kwaribuni ambapo wanasayansi kwa shida sana na kwa kutumia teknolojia ya kisasa iliyoendelea sana wameligundua jambo hilo."

“Mtu ambaye hakuwa akijua chochote kuhusu fizikia za nyuklia miaka 1400 iliyopita nafikiri, kwa kutumia akili yake tu, asingekuwa katika nafasi ya kugundua mathalan kwamba ardhi na mbingu vina asili moja, au masuala mengine mengi ambayo tumeyajali hapa…Ukikusanya pamoja maelezo yote haya yaliyotolewa na Qur’an juu ya mambo yanayohusu ardhi na mpangilio / uumbikaji wa ardhi na sayansi kwa aujumla, kimsingi unaweza kusema kwamba maelezo hayo yaliyotolewa ni sahihi na ni kweli kwa namna mbalimbali, sasa yanaweza kuthibitishwa na utafiti wa kisayansi. Unaweza kusema kwa uwazi kabisa kuwa Qur’an ni kitabu sahihi cha sayansi kwa mwanadamu sahihi. Na kwamba maelezo mengi yaliyotolewa humo hayakuweza kuthibitishwa kwa wakati huo, lakini sasa utafiti unaofanywa sasa hivi wameweza kuthibitisha kile kilichosemwa na Muhammad miaka 1400 iliyopita"
_____________________



Dr. Yoshihide Kozai
Mkurugenzi wa Tokyo Observatory, Tokyo, Japan.
 Dr. Yoshihide Kozai ni Profesa wa Heshima katika Chuo Kikuu cha Tokyo, Hongo, Tokyo, Japan, na alikuwa Mkurugenzi wa Mahali pa kuangalia (jua, mwezi na nyota) Unajimu Kitaifa, Mitaka, Tokyo, Japan. 
Sheikh Abdul-Majeed A. Zindani alimpatia aya kadhaa zinazoelezea mwanzo wa ulimwengu na mbingu, na uhusiano uliopo kati ya mbingu na ardhi. Alielezea kushangazwa kwake, akisema kuwa Qur’an inaielezea dunia kama inavyoonekana kwa mtu anayeitazama kwa upande wa juu, kila kitu kipo wazi na kipo dhahiri.

Alisema:
“Nimevutiwa sana na kwa kukuta ukweli wa taarifa za kinajimu kutoka ndani ya Qur’an, na kwetu sisi, wanajimu wa zama hizi tulikuwa tukichunguza vipande vidogo sana vya ulimwengu. Nguvu zetu tulizielekeza katika kuelewa sehemu ndogo sana. Kwa sababu, kwa kutumia darubini, tunaweza kuona sehemu chache sana ya anga pasi na kufikiri (juu ya) ulimwengu mzima. Hivyo, kwa kuisoma Qur’an na kwa kuyajibu maswali, nadhani naweza kuipata njia ya baadaye kwa ajili ya kuuchunguza ulimwengu.”
_____________________

Profesa Armstrong

Profesa Armstrong anafanya kazi na shirika la anga la Marekani (NASA) na pia ni profesa wa masuala ya anga (Astronomy), Chuo Kikuu cha Kansas, Lawrence, Kansas, Marekani.
Prof. Armstrong aliulizwa maswali kadhaa kuhusu aya za Qur’an zinazohusu fani yake. Aliulizwa:
“Umejionea na kugundua mwenyewe maumbile halisi ya astronomia ya kisasa kwa kutumia chombo cha kisasa, roketi, satellite mbalimbali zilizotengenezwa na mwanadamu. Vilevile umeona jinsi mambo hayohayo yalivyoelezwa ndani ya Qur’an karne kumi na nne zilizopita. Sasa ni yepi maoni yako?”

"Hilo ni suala gumu ambalo nimekuwa nikilifikiria tangu tulipoanza mjadala wetu hapa. Nimevutiwa sana na namna baadhi ya maandiko ya zamani yanavyoafikiana na elimuanga iliyovumbuliwa hivi karibuni. Mimi sio mwanachuoni wa kutosha wa historia ya binadamu kwamba nijiweke moja kwa moja katika mazingira yaliyokuwepo miaka 1400 iliyopita. Kwa hakika, ningependa kuliacha hilo kwamba, kile tulichokiona ni cha ajabu, kikiwa au kisiwe na maelezo ya kisayansi, lazima kuna kitu ambacho kitakuwa nje ya uelewa wetu wa maarifa ya kibinadamu katika kufafanua maandiko ambayo tumeyaona."

_____________________

William Hay


Dr. William W. Hay ni mwanasayansi mashuhuri juu ya masuala ya baharini. Yeye ni Profesa wa Sayansi ya Jiolojia katika Chuo Kikuu cha Colorado, Boulder, Colorado, Marekani. Hapo kabla, alikuwa Mkuu wa Shule ya Rosentiel inayohusika na Masuala ya Baharini (Marine) na Sayansi ya Angahewa katika Chuo Kikuu cha Miami, Florida, Marekani. Baada ya majadiliano na Profesa Hay kuhusu Qur-aan kwamba iliyataja masuala mambo yaliyogundulika hivi karibuni juu ya masuala ya bahari, alisema:
“Ninakuta kwamba ni jambo la kuvuta fikra kwamba khabari ya namna hii imo katika maandiko ya kale ya Qur-aan Tukufu, nami sina njia ya kujua kwamba huenda yamekuja kutoka wapi, lakini inavuta fikra mno kuwa yangalipo na kwamba, kazi hii inaendelea ili igundue, maana ya baadhi ya vifungu vya maneno.” Alipoulizwa kuhusu chanzo cha Qur-aan, alijibu: “Naam, nadhani lazima itakuwa ni Mungu".
_____________________ 

Durja Rao

Profesa wa Jiolojia ya Bahari katika chuo kikuu cha Mfalime Abdulaziz , Jeddah, Saudi Arabia.
Sheikh Zindani alimpatia Prof. Rao aya nyingi zinazohusu eneo la fani yake, na kumuuliza:

 "Unasemaje kuhusu kuwepo kwa taarifa za kisayansi ndani ya Qur'an? Mtume Muhammad aliwezaje kuyajua mambo haya karne kumi na nne zilizopita?"

"Ni vigumu kufikiri kwamba aina hii ya maarifa ilikuwepo zama hizo, takriban miaka 1400 iliyopita. Huwenda baadhi ya mambo walikuwa na taarifa nayo kwa kiwango kidogo, lakini kueleza kwa kina mambo hayo ni jambo gumu sana. Kwa hiyo, maarifa haya hayatokani na mwanadamu hata kidogo. Mwanadamu wa kawaida hawezi kutoa maelezo ya kina kuhusu maajabu haya. Hivyo, naona kuwa taarifa hii lazima itakuwa imetoka kwa chanzo chenye uwezo ulio juu ya uwezo wa chochote.

_____________________

Profesa Siaveda
Profesa wa Jiolojia ya Bahari, Japan.

Sheikh Zindani alimuuliza maswali kadhaa yanayohusu fani yake, na kisha akamueleza kuhusu aya za Qur’an pamoja na hadithi mambo ya kimaumbile aliyoyazungumzia. Swali moja lilikuwa likihusu milima. Sheikh Zindani alimuuliza kuhusu muundo wa milima; na iwapo ilikuwa imewekwa kama vigingi katika ardhi.

"Ni yepi maoni yako kuhusu ulichokiona ndani ya Qur’an na Sunnah kuhsu siri mbalimbali za ulimwengu, ambazo wanasayansi wamezigundua leo?”

"Kwangu mimi laonekana kuwa mwujiza wa hali ya juu, jambo la kuashangaza na la taabu kuaminika. Nadhani kama kweli ulichosema ndicho, kitabu hiki ni cha ajabu mno, ninakubali."

_____________________

Tejatat Tejasen

Profesa Tejatat Tejasen ni Mwenyekiti wa Idara ya Anatomia katika Chuo Kikuu cha Chiang Mai, Chiang Mai, Thailand. Kabla ya hapo, alikuwa Mkuu wa Kitivo cha Tiba katika chuo hicho hicho. Wakati wa mkutano wa nane wa Saudi wa masuala ya tiba jijini Riyaadh, Saudi Arabia, Profesa Tejasen alisimama na akasema:
“Katika miaka mitatu iliyopita, nilijikuta nikivutiwa na Qur’an. ....Kutokana na uchunguzi wangu na kutokana na nilichojifunza katika mkutano huu, naamini kuwa kila kilichoandikwa ndani ya Qur’an mnamo miaka elfu moja na mia nne iliyopita, ni lazima kuwa ni kweli, ambao unaweza kuthibitishwa kwa njia za kisayansi. Kwa kuwa Mtume Muhammad hakuweza kusoma wala kuandika, Muhammad ni lazima kuwa ni Mtume aliyeupokea na kuueneza ukweli huu, ambao ulishushwa kwake kama uongofu kutoka kwa anayestahiki kuwa ni muumbaji. Lazima muumbaji huyu awe ni Mwenyezi Mungu. Hivyo, nadhani huu ndio muda muwafaka wa kusema La ilaaha illa Allaah, hapana mola wa haki kuabudiwa isipokuwa Mwenyezi Mungu, Muhammadur Rasulullah, Muhammad ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu. Mwisho, ni lazima nipongeze kwa mipango mizuri sana na ya mafanikio makubwa ya mkutano huu... Si kwamba nimepata kutoka katika nukta ya mtazamo wa kisayansi na wa ki-Dini lakini pia fursa kubwa ya kukutana na wanasayansi wengi mashuhuri na kupata marafiki wengi miongoni mwa washiriki. Kitu cha thamani kubwa kuliko vyote nilivyopata kwa kuja kwangu mahala hapa ni La ilaaha illa Allaah, Muhammadur Rasulullah, na mimi kuwa Muislamu.”
Baada ya mifano yote hii, tumeona juu ya miujiza ya kisayansi katika Qur’an Tukufu na maoni yote haya ya wanasayansi juu ya hili, hebu tujiulize maswali haya:
  • Inaweza kuwa ni suala la utukizi kuwa maelezo haya ya kisayansi yaliyogundulika hivi karibuni kutoka katika nyanja tofauti tofauti yalikuwa tayari yalishaelezwa katika Qur’an, ambayo iliteremshwa karne kumi na nne zilizopita?
  • Je, inawezekana kuwa Qur’an hii ilitungwa na Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) au mtu mwingine?

_____________________

Dr. Maurice Bucaille

Akiwa amezaliwa mwaka 1920, Mkuu wa zamani wa Kliniki ya upasuaji, Chuo kikuu cha Paris, kwa muda mrefu amekuwa akijishughulisha na kufanya uchunguzi na kufanya mlinganisho baina ya mafundisho ya Maandiko Matakatifu na elimu ya kisasa ya kisekula.

Ni mwandishi wa kitabu kinachonunuliwa zaidi cha "The Bible, The Qur'an and Science" (1976). Usomaji wake wakina wa lugha za maandiko matakatifu, ikiwa ni pamoja na Kiarabu, kwa kuhusisha maarifa yake ya maandiko ya hairoglifu, umemuwezesha kufanya utafiti wa kina, ambapo mchango wake binafsi kama daktari umetengeneza hoja zenye kuondoa shaka. Kitabu chake kiitwacho, "Mummies of the Pharaohs - Modern Medical Investigations" (St. Martins Press, 1990), kilishinda Tuzo ya Historia kutoka Académie Française na tuzo nyingine kutoka Chuo cha tiba cha Ufaransa (French National Academy of Medicine).

Vitabu vyake vingine ni pamoja na: "What is the Origin of Man" (Seghers, 1988), "Moses and Pharaoh, the Hebrews in Egypt", (NTT Mediascope Inc, 1994); and "Réflexions sur le Coran" (Mohamed Talbi & Maurice Bucaille, Seghers, 1989).

Baada ya utafiti uliodumu kwa kipindi cha miaka kumi, Dr. Maurice Bucaille alikihutubia chuo cha tiba cha Ufaransa mwaka 1976 kuhusu uwepo wa maelezo kadhaa ndani ya Qur’an yanayozungumzia fiziolojia na mfumo wa uzazi wa binadamu. Sababu yake ya kufanya hivyo ni:

"...maarifa yetu juu ya misingi hii ni kwamba, haiwezekani kufafanua jinsi maandiko fulani katika enzi za Qur’an yangeweza kuwa na mawazo yamegunduliwa tu katika nyakati za hivi karibuni."

"Uchunguzi huo unaifanya nadharia iliyoibuliwa na wale wanaomuona Muhammad kama mtunzi Qur’an kuwa nadharia dhaifu isiyoweza kusadikika wala kutetewa. Mtu amabaye hakusoma aliwezaje kuwa mtunzi / mwandishi mkubwa, kwa uandishi maridhawa, katika fasihi nzima ya Kiarabu? Kisha aliwezaje kutamka ukweli wa sayansi ya maumbile ambayo hakuna binadamu mwingine aliyeweza kuyavumbua wakati huo, na yote haya aliyaeleza bila kukosea hata kidogo katika uelezeaji wa suala husika?"
Twitter Bird Gadget