Monday, February 13, 2012

Mungu wa nafsi Tatu


NAFSI TATU ZENYE SIFA TOFAUTI KABISA
Kama Mungu Baba, Yesu na Roho Mtakatifu ni nafsi tatu zenye sifa mbali mbali kabisa ambazo katika hizo hazishirikiani zote tatu, hapo hizo tatu haziwezi kuhesabiwa kuwa 'Tatu katika moja' na 'Moja katika tatu'. Utatu unaweza kuunganika ukawa umoja hasa hapo tu ambapo nafsi zote tatu zinakuwa na mienendo ile ile na sifa zile zile na kazi zile zile na nguvu zile zile za aina moja wala hamna hata sifa moja maalum inayoitenga moja na nafsi nyingine mbili. Hiyo inaweza kufananishwa kiasi fulani na watoto watatu waliozaliwa kutokana na mimba moja ambao wanafanana sana sana kabisa, hata fikra zao, maono yao na kazi za viungo vyao vinaafikiana mno hata kwamba majaribu ya kila mmoja wao ni majaribu ya wote hao kikamilifu  bila tofauti yoyote.
 
Kama ndivyo ilivyo, hapo Utatu wa Mungu, Mwana na Roho Mtakatifu utaweza kueleweka zaidi. Lakini bado tatizo litabaki kuhusu miili mitatu yenye nafsi hizo tatu zinazofanana kwa kila jiha kikamilifu. Lakini hiyo haiafikiani na wazo la Kikristo juu ya Utatu. Mtu akiangalia mara ya pili analazimika kuwaza picha ya mwili mmoja wenye nafsi tatu mle ndani. Lakini umoja huo wa watatu unaweza kuzingatiwa hapo tu ambapo mwili mmoja ukiweza kuwa na nafsi tatu ndani yake, jambo ambalo linazua matatizo mengi. Naam, kwa kuwa Mungu hana mwili, kwahiyo mithali ya mwili wa kibinadamu ilivyoshauriwa nyuma haifai. Twajua sana ya kwamba Mungu hana mwili, lakini bado tatizo litabakia kuhusu Ukristo - Safari  kutoka  Hakika  kuelekea  kwenye Ubunifudhati tatu za kiroho zilizo kama wale watatu waliozaliwa kutokana na mimba moja wanaofanana, wanaokuwepo mbalimbali lakini wanaungana katika mambo mengine yote. Tatizo jingine litakalowakabili hao watatu wa kukisiwa ni namna wanavyohusiana wao kwa wao katika habari ya ibada. Je, nafsi zote tatu za 'Tatu katika Moja' zinaabudiana zenyewe kwa zenyewe? Je, zote hizo zinapokea ibada za viumbe vyao, lakini haziabudiani zenyewe kwa zenyewe?
Ingawaje Yesu Kristo anatajwa mara kwa mara katika Agano Jipya akimwabudu Mungu Baba na anawasihi wengine pia kumwabudu Yeye.

Lakini haikuelezwa kuhusu Roho Mtakatifu akimwabudu Mungu Baba. Tena hamna kabisa habari ya Yesu k u j a r i b u   k u w a e l e k e z a   w e n g i n e   k u m w a b u d u   y e y e   w a l a
kumwabudu Roho Mtakatifu sawa na taarifa ya Agano Jipya. Mtu anakanganywa na kutokutajwa kuabudiwa kwa Yesu na Roho Mtakatifu katika Agano Jipya, lakini habari ya Mungu Baba kuabudiwa imetajwa mara kwa mara.

Ijapokuwa ni desturi ya kawaida ya Wakristo kumwabudu Yesu kuwa 'Mwana wa Mungu' pamoja na kumwabudu Mungu Baba, hata hivyo hamna taarifa yoyote iliyohifadhiwa katika maandiko ya  kwamba  mwana funz i  yeyot e  wa  Ye su Kr i s to  a l iwahi kumwabudu yeye, ama Yesu akawaelekeza kufanya hivyo katika muda wote aliokaa ardhini. Hata kama yeye angelifanya hivyo, maswali mengi yasiyoweza kujibika yangezuka.
Ndivyo ilivyo hali ya Roho Mtakatifu, yeye naye hakumtaka yeyote kumwabudu yeye. Kwa nini? Ile hali imekwisha chunguzwa tayari kiasi fulani ambako hao walikuwa 'Tatu katika Moja' katika maana hii ya kwamba u t amb u z i  wa o  wa   k uwa p o   kwa o   u l i k uwa  mmo j a   j u u   y a kugawanyika katika hali ama jiha tatu. Dhati ya aina hiyo haiwezi kiakili kuhesabiwa kuwa 'watu watatu katika mmoja'. Aidha, hali ama jiha haziabudiwi, wala hazijiabudu. Kwa kuwatambua kuwa watu watatu tofauti, wanalazimika kujijua wanakuwapo kwa Utatukujitegemea. La sivyo, suala la kujitaja ama kuwataja wengine kwa kusema 'Mimi', 'Wewe' na 'Yeye' halizuki asilani.
 
Utatu ukitumika kwa dhati moja humaanisha sifa tu basi. Na sifa kwa kweli hazina kikomo, haziwezi kuwa tatu tu. Tujue tusijue, Mungu anazo sifa nyingi teletele. Kwa kumalizia mazungumzo haya, twasisitiza mara nyingine ya
kwamba suala la wao kuabudu wao kwa wao linaweza kuzuka hapo tu ambapo hao wangekuwa watu watatu wenye madaraka mbalimbali na sifa tofauti. Katika shauri hiyo, mmoja tu ataabudiwa na wengine wawili wakiwa wenye daraja dogo watatazamiwa kumwabudu yeye. Hilo lakubaliwa, lakini ule 'Umoja katika utatu' utatoweka. Hamna njia yoyote ya kuwa na 'Tatu katika Moja' na 'Moja katika Tatu', zote mbili hizo, wakati huohuo mmoja. Hiyo imenikumbusha kisa kimoja cha kuchekesha ambacho ningependa kuwaambieni. Imesimuliwa ya kwamba wakati Tamerlane alipovamia mji wa Baghdad alifurahiwa na Bwana Joha, mcheshi wa mahakama, mpaka akaamua kumchukua pamoja naye kama mateka na akampa kazi maalum ya kuwa mchekeshaji mkuu wa korti. Inasemekana safari moja Joha aka j awa  na   shauku ya  kul a  nyama   akiwa  peke  yake  bi l a kushirikiana na wengine. Akashikwa na kiherehere hicho sana hadi hakuweza kujizuia. Basi akanunua nyama kilo mbili nzuri kabisa kutoka kwa muuza nyama. Alipomkabidhi mkewe nyama hiyo akaagiza kuichoma vizuri sana, lakini akamuambia hakuna atakayeila isipokuwa yeye peke yake, yaani Joha, hata mkewe hawezi kuionja. Sasa kwa bahati mbaya, mkewe alipokwisha tu kuichoma vizuri sana nyama hiyo, ghafula wakaja nduguze kadha kumtembelea. Hiyo ilikuwa furaha aliyopata ghafula, lakini ikawa habari mbaya ya kwa Joha.

Harufu nzuri ya kuvutia iliwashinda hao ndugu za mkewe, na matokeo ndiyo unaweza kukisia. Wakala na  kumaliza mpaka kipande cha mwisho kisha wakamwaga dada yao ambaye sasa akaanza kuhangaika. Lakini akajituliza kabla h a j a w a s i l i   n y u m b a n i   B w a n a   J o h a ,   m a a n a Ukristo - Safari  kutoka  Hakika  kuelekea  kwenye Ubunifualishawaza hila ama udhuru fulani ili kujiokoa katika hali hiyo ngumu. Joha alipoingia na akasikia harufu nzuri ya kuvutia ya nyama iliyochomwa ambayo ilikwisha liwa tayari, akamwagiza mkewe kuleta haraka hiyo nyama.
Hapo mkewe akiashiria kwenye paka wa Joha aliyekuwa amemfuga kwa shauku sana, akasema:
Toa nyama yako kutoka katika paka huyu, ukiweza.  

Maana nilipokuwa nimeshughulika, huyu akaila yote. Hapo haraka sana Joha akamshika paka na kumpima katika mizani. Kumbe uzito wake ulikuwa kilo mbili barabara. Basi kamwelekea mkewe kwa upole na akamuuliza: Mke wangu mpenzi, hakika nimekubali ulivyosema, lakini kama hiyo ndiyo nyama yangu, basi yuko wapi paka wangu; na kama huyu ndiye paka wangu, basi nyama yangu iko wapi!

Achilia mbali vichekesho, nisingependa kujadili suala hilo juu ya msingi wa mafunzo halisi na ya kweli ya Yesu. Maandiko haya shabaha yake hasa ni kuchunguza itikadi za sasa hivi za Kikristo ambazo twaamini kwamba zimepotoka na kwenda mbali kabisa na mafunzo ya asili ya Yesu. Tukiisha kanusha habari ya Yesu kuabudiwa ndani ya Biblia, inatulazimu kufafanua sehemu ya pekee ndani ya Biblia, yaani Luka 24:52 ambamo Yesu anaonekana aliabudiwa. Wengine wanasema ya kuwa mstari huo unatoa ushahidi ya kwamba Yesu aliwahimiza kumwabudu. Wataalamu wa Kikristo wa zama hizi wanaelewa sana ya kwamba mistari hiyo imekwisha hakikishwa kuwa ya uwongo iliyoongezwa baadaye wala hakuna haki ya kuihesabu mistari hiyo kuwa sehemu halisi ya Injili ya Mt. Luka. Hebu sasa tugeukie kwa suala la desturi ya kawaida kwamba je hiyo inathibitika kwa ushuhuda uliomo katika Injili ama hapana. Sawa na desturi ya kawaida, Yesu anaabudiwa akiwa 'Mwana wa Mungu' katika madhehebu mengi ya Kikristo.

Hata hivyo wote hao wanakiri ya kwamba Yesu huyohuyo mwenyewe alikuwa
anamwabudu Mungu Baba peke yake. Bure kabisa nimewauliza mara nyingi wataalamu wa Kikristo wenye ujuzi mwingi ya kwamba kwa nini Yesu alimwabudu UtatuMungu Baba ikiwa yeye mwenyewe alikuwa sehemu ya Mungu isiyoweza kutenguka na alikuwa ameunganika naye kabisa kikamilifu kwa kuleta maana ya umoja japo nafsi tatu zilikuwepo? Je siku yoyote aliwahi kumwabudu Roho Mtakatifu pia aliye nafsi ya tatu katika Utatu? Je, alijiabudu wakati wowote? Je, Roho Mtakatifu alimwabudu Yesu siku yoyote? Na je, Baba aliwahi siku yoyote kumwabudu yeyote miongoni mwa wawili wengine wa Utatu?  Kama hapana kwa nini? Pengine majibu ya suala hilo yatawalazimisha Wakristo kukiri ya kwamba Baba anacho cheo kikubwa zaidi kuliko nafsi mbili nyingine za Utatu.
Inathibitika kutokana na hiyo ya kwamba sehemu tatu za Utatu haziko sawa katika daraja. Hivyo, hao ndio 'Watatu katika Watatu' kama kwa vyovyote wako watatu, lakini siyo kabisa 'Watatu katika Mmoja'. Wakati mwingine wataalamu wa Kikristo wanapokabiliwa na swali  la Yesu, wanayemwamini kuwa Mwana wa Mungu, k u m w a b u d u   M u n g u   B a b a ,   h u s e m a   Y e s u - m t u   n d i y e aliyemwabudu Mungu Baba, siye Yesu Mwana aliyemwabudu Yeye. Hiyo inatupeleka nyuma tena kwenye mazungumzo tuliyokwisha fafanua tayari. Je, mwili huohuo mmoja wa Yesu ulikaliwa na nafsi mbili, moja yenye dhamira ya binadamu na nyingine ya Mwana wa Mungu?

Aidha, kwa nini mtu ndani ya Yesu aliepa na kumpuzilia mbali kabisa Mwana wa Mungu aliyekuwemo ndani yake asimwabudu Kr i s to ha t a  ma r a  moj a ?  Huyo huyo Ye su-mtu  a l i t akiwa kumwabudu Roho Mtakatifu pia aliye nafsi ya tatu katika Utatu, lakini mbona hakufanya hivyo katu! Ibada ni tendo la moyo na roho ambalo pengine huoneshwa kwa alama za kimwili, lakini lina mizizi yake katika fahamu na maono ya dhamiri  ya mtu. Hivyo inapaswa  kungunduliwa nani aliabudu pindi Yesu Kristo alipomwabudu Mungu. Tumekwisha eleza
jambo hilo hapo kabla pamoja na matatizo yake ya kwamba Kr i s to,  Mwana  wa  Mungu,  ndiye   a l iyemwabudu Mungu.
 
Kinyume chake, kama alikuwa ni mtu aliyemwabudu Mungu Baba, na huyo mtu hakumwabudu Kristo, kwa nini basi Wakristo Ukristo - Safari  kutoka  Hakika  kuelekea  kwenye ubunifuwanaukaidi mfano huo bora wa Yesu mwenyewe? Kwa nini wanaanza kumwabudu Kristo pamoja na Mungu, ilhali Yesu-mtu hakumwabudu mwenzake Kristo japo alikaa karibu yake mno.

NAFSI TATU ZENYE SIFA ZIFANANAZO ZILIZO SAWA:
Hebu tuchunguze mara nyingine tena, lakini safari hii kwa jiha tofauti kabisa, kanuni ya 'Tatu katika Moja' ndani ya Utatu, tukizichukua kuwa dhati tatu tofauti lakini zenye sifa zilezile zifananazo kabisa kikamilifu. Hapa hatuzungumzii dhati moja yenye sifa mbalimbali zilizounganika pamoja, bali twazungumzia dhati tatu kama watoto watatu waliozaliwa katika mimba moja.

Twazungumzia hao watatu ambao wanafanana wao kwa wao sana kabisa hata kwamba kufanana kwao hakuishii tu katika kufanana umbo na sura, bali hata fikara zao na maono yao pia ni ya aina moja. Wanashirikiana katika fikira zao, maono yao na majaribu yao kwa namna moja kabisa. Hapo mtu hana budi kukiri ya kwamba nafsi mbili katika utatu hazina kazi tena, ni bure kabisa. Kama hizo mbili zikiondolewa mbali, hazitaleta kasoro yoyote
ile iwayo kwa nafsi iliyobaki ya Utatu ambayo nafsi hiyo itakuwa kamilifu peke yake.

Quran Tukufu pia inauliza swali hilo inapodokeza ya kwamba kama Mungu akiamua kumuangamiza na kumfutilia mbali kabisa Yesu Kristo na Roho Mtakatifu, tofauti gani itatokea kwa utukufu wake, Umilele wake na Ukamilifu wake, na ni nani awezaye kumzuia Yeye asifanye hivyo (5:18). Hiyo inamaanisha ya kwamba sifa zote za Mungu zitaendelea kufanya kazi milele na kwa hivyo itikadi ya Utatu ilivyoelezwa hivi sasa haina maana wala haihitajiki Utatu

Lakini kama ifikiriwe ya kwamba dhati tatu hizo za utatu zinafanya kazi mbalimbali, hapo bila shaka sehemu zote tatu za utatu zitahitajika ili kufanyiza Mungu. Hata hivyo hapo patakuwa na Miungu watatu tofauti wanaosaidiana wao kwa wao na kukaa pamoja kwa amani kamilifu na hapo wanaweza kuhesabiwa 'Miungu Watatu katika Watatu' wala hapana 'Miungu Watatu katika Mmoja'. Na kama isemwe ya kuwa Utatu ndiyo kama mtu mmoja mwenye viungo mbalimbali vinavyofanya kazi tofauti vikiunganika ndani ya mtu mmoja, hapo bila shaka Umoja utakuwepo lakini Utatu utatoweka. Lakini tukumbuke ya kwamba hatuzungumzii hapa
mtu mmoja mwenye viungo kadha vinavyofanya kazi, bali watu watatu wanaofanana kabisa kwa kila hali na kila jiha, na kila mmoja akifanya kazi hizohizo za aina moja na hata hivyo kila moja anabaki kuwa mtu binafsi peke yake. Iliyojadiliwa ni hali ya mtu mmoja mwenye viungo kadha. Mpaka hapo sawa, hamna kilicho kinyume cha akili.

Lakini viungo vikihesabiwa kuwa watu na palepale watu hao wote wakiwa pamoja wanafanyiza mtu mmoja kwa jumla, hapo habari hiyo inakuwa kinyume cha akili wala haiwezi kukubalika. Ni sawa kuwa kila kiungo kina kuwapo kwake, lakini kuwapo huko ndiyo sehemu tu ya mtu ambaye si tu kwamba anacho kiungo hicho tu kimoja bali anavyo viungo vingine pia. Viungo hivyo vikiwa pamoja ndani ya mtu huitwa 'mtu' kwa jumla. Naam, baadhi ya viungo vinafanya kazi ya muhimu zaidi na vingine vina kazi si ya muhimu sana, na mtu anabaki kuwa mtu bila ya viungo hivyo vyenye kazi isiyo muhimu, lakini mtu huyo atakuwa si mkamilifu, bali atakuwa na kasoro fulani. Mtu mkamilifu hupaswa kuwa na viungo vyote vile anavyokuwa navyo mtu yeyote kikawaida, na jumla ya viungo hivyo hufanyiza mtu mkamilifu.
 
Tukichukua mfano wa mtu mmoja aitwaye Paulo, mtu hawezi kusema ya kwamba kwa kuwa ini, moyo, mapafu na mafigo ya Paulo ni vitu maalum mbalimbali ambavyo vina kazi mbalimbali, Ukristo - Safari  kutoka  Hakika  kuelekea  kwenye Ubunifubasi kwa hiyo hivyo ni nafsi mbalimbali zilizokamilika ambazo kila nafsi katika hizo ni sawasawa na Paulo. Kila kiungo chaweza kuwa Paulo hapo tu ambapo kwa mfano mafigo peke yake yafanye kazi zote kwa jumla anazofanya Paulo, na kadhalika kila kiungo kiwe hivyo hivyo. Jambo hilo linamaanisha ya kwamba viungo hivyo vikikosekana, hakuna badiliko litakalotokea katika Paulo. Au tuseme kwamba Paulo bado atabaki kuwa Paulo kikamilifu kama viungo vyake yaani mapafu, moyo, mafigo na ubongo, kwa hakika viungo vyote vikiondolewa mbali. Hiyo ni kwa sababu katika ukaguzi wa mwisho viungo hivyo vyote vinafanana, na dhati ya Paulo inabakia tu pale pasipo kujali viungo hivyo vipo ama havipo.

No comments:

Post a Comment

Twitter Bird Gadget