TIPPU TIP

Akiwa ametiwa ila sana na "magazeti ya wavumbuzi," shujaa huyu jasiri wa kizanzibari ambaye jina lake hasa aliitwa Hamed bin Mohammed Marjebi alijulikana zaidi kama Davy Corocket au Francis Drake wa Afrika ya Mashariki kuliko mfano wa mwanafunzi mtundu ambaye tabia zake zilizompa umaarufu zaidi ni vile kuwa na ugomvi wa mara kwa mara na wavumbuzi wa kidini kutoka Ulaya wa wakati ule. Aliwatumikia Sultani wake kwa zaidi ya miaka 50, huku akibeba bendera na ustaarabu wao katika kila pembe ya mipaka yao.
Katika nyakati tafauti, alifanya kazi kama mvumbuzi, kiongozi, mfanyabiashara, askari mwanadiplomaisa, hakimu na gavana. Aliwatumikia jumla ya Sultani 8 wakati wa maisha yake baadaye akastaafu na kubakia nyumbani kwake katika Mji Mkongwe. Alifariki mwaka 1905 akiwa hakuwahi kuhalifu kazi zote alizopewa na watawala wake.
SITI BINTI SADI.

Akiwa mtoto wa watumwa, Siti alianza maisha kwa akali ya kitu, lakini kwa juhudi yake mwenyewe na sauti yake ya ajabu, aliweza kwanza kuimba taarabu ya kawaida, baadaye katika makasri na kumsifu Mfalme, na hata kuimba kwa Kiarabu. Baadaye aliigeuza midundo na mifumo ile ya kishairi na kuwa katika vinanda vya kawaida. Matokeo yake, Taarab ya Kiswahili ilimfanya awe Nyota na yeye kuifanya taarab iwe aina ya sanaa ambayo bado ni maarufu visiwani na isiyokosekana katika harusi na sherehe zote za Kizanzibari ..
BARGHASH BIN SAID

Pengine alikuwa Sultan wa mwisho kuweka kipimo cha uhuru wa kweli dhidi ya udhibiti wa Wazungu. Alishauriana na "Washauri" kadhaa wa kizungu ambao walikuwa na ushawishi mkubwa, lakini alibaki kuwa mtu imara waliyepambana naye kumdhibiti alipambana na wanadiplomasia kutoka Uingereza, America, Ujerumani, Ufaransa na Ureno na mara kwa mara aliweza kuiangusha kitaalau nchi moja baada ya nyengine katika kinyang'anyiro cha kabla ya Ukoloni. Ni mtoto wake, Khalid, ambaye katika mchuano wa kurithi ufalme, alishindwa katika Vita vifupi kabisa katika histora.
SHEIKH ABDALLA SALEH FARSY

Sheikh Abdulla aliteuliwa kuwa Mkaguzi Mkuu wa shule za msingi za Unguja na Pemba mnamo mwaka 1949, Mkuu wa Shule ya Lugha ya Kiarabu mwaka 1957 na Kadhi Mkuu wa Zanzibar mwak 1960. Aliondoka visiwani baada ya Mapinduzi ya 1964 na akafia Omani Novemba 9 mwaka 1982.
TARIA TOPAN

Kwa utajiri wake huu, Topan aligeuka kuwa mfadhili Mkuu wa mji. Aliweka Wakfu na kujenga Kituo cha Afya kilichonakishiwa ambacho kipo Kaskazini kabisa mwa Bandari ya Mji Mkongwe. Vile vile alitoa "Wakf" vikataa vya ardhi vilivyokusudiwa kuwanufaisha wazee wasiojiweza.
NAHODHA "SMITH WA ZANZIBAR"
Wamarekani wao waliuza nguo za pamba (Mrekani) na kununua vipusa, viungo na sandarusi ambayo ilitumika kutengeneza vanishi kwenye viwanda vya New England. Kwa kufanya biashara na Marekani, kuliifanya Zanzibar kuwa kituo Kikuu cha Biashara katika maeneo haya.. Hata kufikia mwaka 1830, katika kipindi cha miezi 18, jumla ya vyombo 32 kutoka Amerika vilishatia nanga katika bandari ya Zanzibar.Mnamo mwaka 1836 kiwango cha biashara baina ya nchi mbili hizi ilihakikisha kuanzishwa Balozi za Amerika za kudumu katika Mji Mkongwe. William Smith alisafiri "kuzunguka pembe" ya Afrika mara nyingi katika safari ndefu za kutoka Amerika na visiwani kiasi cha kujulikana kama Smith wa Zanzibar katika pande zote za ikweta
No comments:
Post a Comment