Monday, February 20, 2012

Dua ya maumivu


Dua ya kusma Muislamu anapopata maumivu katika mwili wake.

 عنعثمان بن أبي العاصأنه شكا إلى رسول الله  صلى الله عليه وسلموجعا يجده في جسده , فقال له رسول الله  صلى الله عليه وسلم: ((ضع يدك على الذي يألم من جسدك وقل بِسْمِ اللهِ  ثلاثا وقل سبع مرات:   أَعُوذُ باللهِ وَقُدْرَتِهِ مَنْ شَرِّ مَا أَجِدُ وَأُحَاذِرُ))  رواهمسلم
Kutoka kwa 'Uthmaan bin Abil-'Aasw kwamba alilalamika kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) maumivu aliyopata mwilini mwake, akasema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ((Weka mkono wake sehemu inayokuuma katika mwili wako na useme: BismiLLaah mara tatu, kisha sema mara saba: A'uudhu BiLLaahi wa Qudratihi Min Sharri Maa Ajidu wa Uhaadhiru[Najilinda kwa Allaah na kwa uwezo Wake kutokana na shari ya ninachokisikia na ninachokiogopa])) [Muslim]

Ama kumswalia Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mara mia na kumpulizia, hatukupata dalili katika mafunzo yetu, ikiwa ni kwa ajili ya kuondosha maumivu au hata kwa kutaka tu fadhila zake.

No comments:

Post a Comment

Twitter Bird Gadget