Friday, April 6, 2012

HESHIMA YA MWANAMKE KATIKA UISLAMU


Ndugu katika imani, suali la mwanamke ni suali ambalo liliwashughulisha watu wengi walio pita, na linendelea kuwashughulisha wengi katika zama zetu hizi. Dini na mila mbalimbali zimezungumzia hali ya mwanamke katika jamii. Wasomi wa ilimu na falsafa tafauti wamejaribu kuzugumzia cheo cha mwanamke katika jamii. Lakini kila kundi linajaribu kuzungumzia mwanamke kwa misingi ya kufikia malengo yao. Katika khutba hii tutajaribu kuangazia cheo cha mwanamke katika jamii mbalimbali. Tutangalia hali ya mwanmke kabla ya kuja Uisalmu, na haliyake katika Uisalmu, na haliyake katika mataifa ya magharibi.
Hali ya Mwanamke kabla ya kuja Dini ya kiislamu
Alikuwa mwanamke katika zama za ujinga akionekana kama bidhaa ambao haina thamani. Kila mtu anaweza kumiliki bidhaa hio wakati wowote. Wanaume wakiowa wanawake bila ya idadi maulumu na kuacha bila ya idadi ya talaka. Mwanamke haruhusiwi kumiliki chochote, hana haki ya kurithi, anaweza kuolewa na zaidi ya mume mmoja. Mwanamke hakuwa na cheo katika jamii ya ujahiliyah, bali alikuwa akionekana ni mtu anaye leta  aibu katika jamii. Ikafikia hali hio, baaadhi ya wanaume kuwazika mabanati wao wakiwa wadogo kuogopea kuleta aibu katika jamii. Mwenyezi Mungu (SW) Anatueleza hali ya mwanamke Akisema:
قال تعالى: {وإذا بشر أحدهم بالأنثى ظل وجهه مسودا وهو كظيم. يتوارى من القوم من سوء ما بشر به أيمسكه على هون أم يدسّه في التراب ألا ساء ما يحكمون}
{{ Na mmoja katika wao anapopewa khabari ya kuzaliwa mtoto wa kike, unabadilika uso wake huwa mweusi na akajaa sikitiko. Anajificha na watu kwa sababu ya khabari mbaya ile alioambiwa. (anafanya shauri) Je, akae naye juu ya fedheha hiyo, au amfukie udongoni. Ni mbaya mno hukumu yao hiyo}}. Hii ndio hali halisi ya mwanamke kabla ya kuja Dini ya kislamu. Na hali hii ilikuwa sawa katika  mataifa yote, sawa taifa la kiarabu na wasiokuwa waarabu.

Hali ya Mwanamke katika Uisalmu
Baada ya mwanamke kuishi katika dhulma kwa mda mrefu, bila ya kupata haki zake. Allah (SW) Alimtumiliza Mtume (SAW) wake kuja kumkomboa mwanamke na dhulma na udhalilifu alikuwa akipata kutoka kwa jamii anayo ishi. Dini ya kislamu inamtukuza mwanamke na inampa haki zake zote katika jamii. Miongoni mwa haki hizo”-
 قال تعالى: {من عمل صالحا من ذكر أو أنثى وهو مؤمن فلنحيينه حياة طيبة ولنجزينهم أجرهم بأحسن ما كانوا يعملون}
{{ Wafanyaji mema, wanaume au wanawake, hali yakuwa ni Waislamu, tutawahuisha maisha mema, na tutawapa ujira wao mkubwa kabisa}}. Na Mwenyezi Mungu (SW) alimfadilisha mwanamume kuliko mwanamke katika baadhi ya mambo, kwasbabu ya majukumu mazito ya mwanamume katika kusimamia familiya.
وقال سبحانه : { للرجال نصيب مما ترك الوالدان والأقربون وللنساء نصيب مما ترك الوالدان والأقربون مما قل منه أو كثر نصيبا مفروضا}
 {{ Wanaume wana sehemu katika mali wanayoyacha wazazi wao na jamaa waliokaribu. Na wanawaake pia wanayo sehemu katika yale waliyayacha wazazi wao na jamaa waliokaribu. Sawa yakiwa kidogo au mengi. Ni sehemu zilizofaridhishiwa (na Mwenyezi Mungu)}}.
Haya ni baadhi ya mambo muhimu mabao mwanamke amepewa katika Dini ya kislamu. Na hii ndio halihalisi ya mwanamke katika Uislamu. Uislamu ilimrejeshea mwanamke haadhi na utukufu wake katika jamii, na ikatambua mchango wake mkubwa katika kuandaa kizazi cha kesho na kulea viongozi wa kusimamia Dini ya kislamu. Amesema Mtume (SAW) katika Hija: [ Mcheni Mwenyezi Mungu katika kuwasimamia wanawake, kwasababu wao ni wasaidizi wenu]. Mtume anaweka wazi cheo cha mwanamke nacho ni wasaidizi wa wanaume, sio mtumwa au mtumishi  kama wanavyomdai watu wengine kwamba uislamu umefanya mwanamke kuwa ni mtumwa hana haki yoyote katika jamii.
Enyi waja wa Allah, tumcheni Allah na tufanyeni bidii kuwasimamia wake zetu kulingana na alivyo tufundisha Mwenyezi Mungu (SW).

Ndugu Waislamu, na wausieni na kujiusia nafsi yangu kumuogopa Allah (SW), kwani wachaji Mungu ndio wenye kufaulu. Ndugu katika imani, tuangalieni hali ya mwanamke katika nchi zilizoendelea kama wanavyo dai nchi za kikafiri.

Hali ya Mwnamke katika nchi za kikafiri.
Hakika hali ya mwanmke katika nchi hizi ni mbaya sana kushinda hali ya mwanamke katika zama za jahiliyah. Mwanamke amefanywa na kivutio wa kila badhaa au biashara kwa kudhihirisha uchi wake bila ya kujali wala kuona haya. Kila tukiangalia  runinga, kusoma magazeti, internet tunashuhudia mwanamke ndiye wakwanza kuonyesha hali akiwa uchi kabisa kwa lengo la kuvutia watu katika biashara hio. Kwa kweli mwanamke amepokonywa haki zake zote za kimsingi, haki ya kusimamia majukumu ya nyumba, kulea watoto, kuandaa familya juu ya misingi ya tabia njema na maadili mazuri.
 Leo mwanamke hana nafasi nyumbani, kazi yake kubwa nikutoka nje na kwenda kushindana na wanaume, na kudai haki za wanaume katika kazi. Imekuwa hakuna tafauti baina ya mume na mke. Na hili ndilo lengo kubwa la makafiri kumtowa mwanamke nje na kumvunjia hishima yake aliopewa na Allah (SW). Na baadhi ya wanawake wakislamu wameathirika na tabia mbaya za makafiri. Wakaona haya ndio maendeleo na kuenekana umeendelea.
Ndugu waumini, ni wajibu wetu kama wazazi kuwatahadharisha wake zetu mabanati wetu na kasumba mbaya za makafiri. Na tujuwe makafiri hatokuwa radhi mpaka tufuate mila zao. Amesema Mwenyezi Mungu (SW):
قال تعالى: { ولن ترضى عنك اليهود ولا النصارى حتى تتبع ملتهم قل إن هدى الله هو الهدى ولئن اتبعت أهوائهم بعد الذي جاءك من العلم مالك من الله من ولي ولانصير  }
{{ Hawatukuwa radhi juu yako Mayahudi wala Wakristo mpaka ufuate mila yao. Sema hakika uwongozi wa Mwenyezi Mungu ndio uwongozi wa sawa. Na kama ukifuata matamanio yao baada ya yale yaliyokufikia ya ujuzi, hutapata msaidizi yoyote wala mlinzi kwa Mwenyezi Mungu}}.
Mwisho ndugu Waislamu, tukumbuke malipo na fadhila atakazo pata mwenye kumlea msichana malezi ya kislamu kisha amuuzeshe mume mwenye taabia njema basi huyo amedhaminiwa kuingia peponi. Amesema Mtume (SAW): [ Mwenye kuruzukiwa mabinti wa tatu, na akasubiri juu ya kuwalea, kwahakika mtu huyo amewajibika kuingia peponi. Akasema mtu kumuuliza Mtume: vipi ukiwa na wasichana wawili?. Akasema Mtume na wawili pia ni sababu ya kuingia peponi].Ndugu waumini, angalieni rehma ya Allah juu yetu katika kusimamia majukumu ya Allah kwa kuwalea wasichana kwa maadili mema na tabia njema, Allah atakulipa pepo yake ambayo sirahisi ya kuingia kila mtu, ispokuwa watakao simamia majukumu hayo.
Tunamuomba Allah atuafikie tuweze kutekeleza majukumu yote kwa njia ya kumridhisha yeye peke yake. Na tunamuomba Mwenyezi Mungu awahifadhi watoto wetu na kila shari ilio dhahiri na siri.

No comments:

Post a Comment

Twitter Bird Gadget