Friday, April 6, 2012

TAHADHARI NA FITNA ZA WANAWAKE

Leo Mwanamke amekuwa ni bidhaa isiyo na thamani. Kila mtu anaweza kununuwa bidhaa hio kwa thamani ndogo kabisa kwa lengo la kujistarehesha, Mwanamke ni fitna kubwa katika jamii, pindi akijiweka mbali na mafundisho ya Allah. Jamii nyingi zina haribikiwa kwasababu ya maadili na tabia mbaya za wanawake. Athari ya Mwanamke ni kubwa sana katika jamii na kwa Umma wote. Katika Khutba ya leo tutaangazia suali hili muhimu la Fitna za wanawake, na jukumu la Waislamu katika kupambana na fitna hizo.
Mwenyezi Mungu ametuusia sisi na watu waliotangulia kumcha yeye. Na ushahidi wa hayo. Amesema Mwenyezi Mungu (SW)  katika Quraan tukufu:

 {{ Na ni vya Mwenyezi Mungu vyote vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini, na kwa hakika tuliwausia waliopewa kitabu kabla yenu, na nyinyi pia kwamba mumche Mwenyezi Mungu na mkikufuru hakika ya Mwenyezi Mungu ni vyake vilivyomo mbinguni na ardhini na Mwenyezi Mungu ni mkwasi na mwenye kusifiwa}}. Amrisho hilo la kumcha Mwenyezi Mungu ni kwa wote wanaume na wanawake. Lakini kwa vile wanaume ndio wasimamizi wa wanawake inapaswa juu yao kuwalazimisha wake zao juu la suala la kumcha Mwenyezi Mungu kwa njia yoyote ile iliopaswa kisheria. Ushahid wa haya; Anasema Allah (SW):

{{ Wanaume ni wasimamizi wa wanawake kwa vile walivyofadhilishwa na Mwenyezi Mungu baadhi juu ya baadhi na kwa mali wanayotoa}}. Na yote hayo ispokuwa kwa sababu za kimsingi kama utoaji na utazamaji wao wa mambo kibusara. Amesema Shankiti: Mwenyezi Mungu ameashiria kua mwanamume ni mbora kuliko mwanamke kutokana na utukufu na ukamilifu alionao, na mwanamke ana upungufu wa kimaumbile kutokana na kujipamba.
Inafahamika kua wanawake waliokuwa katika zama hizi wanatofautiana na wanawake wa zama za Mtume (SAW). Mbali na wanawake wetu hawatafautiani na wanawake wasiokuwa na dini na kukhalifu miongozo ya dini kwa mfano:
b) -  Kutangamana na wanaume katika vyuo vikuu
Vyote hayo yameharamishwa na ushuhuda wa hapo ni pindi alipotoka Musa na kuelekea Madyana kufika kisimani alikuta pote la watu wanaywesha wanyama wao na akawakuta wanawake wawili wanazuia wanyama wao wasitangamane na wanyama wengine. Akauliza sababu ya kufanya jambo hilo. Wakasema hatunyweshi sisi mpaka wamalize hao kunywesha (yote hayo ni kutokana na unyonge wetu na kutopenda kutangamana na watu).
 Amesema Mwenyezi Mungu kusimulia tukio hilo ndani ya Quraan tukufu:“ Na alipoyafikia maji ya Madyana alikuta umati wa watu wanaywsha (wanyama wao) na akakuta karibu yao wanawake wawili na wanyama wao akawauliza mna nini? Wakasema hatunyweshi sisi mpaka wamalize hao kuchunga, na baba yetu sisi ni mzee sana”. Zingatieni msimamo huo ulinganishwe na yanayo fanyika leo.

 Na katika hadith ya Mtume (SAW):  [ Waamrisheni watoto wenu kusali hali wakiwa na umri wa miaka saba, na wapigeni wakifika miaka kumi na watenganisheni katika malazi]. Hadith hii inamaanisha kutengamana kati yaa mwanamume na mwanamke.
Na miongoni mwa ukiukaji wa maaadili ya kiislamu ni wanawake kudhihirisha mapambo yao jambo amblo linapelekea katika uasharati na kwani Mwenyezi Mungu kaamrisha kuvaa hijabu, kuhifadhi macho na kukataza kujishaua na kudhihirisha mapamabo yake. Amesema Mwenyezi Mungu (SW):
 {{ Na waambie waumini wanaume wainamishe macho yao na wazilinde tupu zao, wala wasionyeshe uzuri wao kwa unao dhihirika, na waangushe shungi zao kwa mpaka vifuani  mwao, na wasionyeshe mapambo yao ila kwa wanaume zao, au baba zao, au baba za waume zao, au watoto wao, au watoto wa waume zao,au kaka zao,au wana wa kaka zao, au wana wa dada zao, au wanawake wenziwao,  au wale ilyowamiliki mikono yao ya kiume au wafuasi wanaume wasio na matamanio, au watoto ambao hawajajua mambo yaliyokhusu ukwe wala wasipige miguu yao ili yajulikane wanayoyaficha katika mapambo yao. Na tubuni nyote kwa Mwenyezi Mungu, enyi waumini ili mupate kufanikiwa}}.
Wamesema wanazuoni: macho ndio mlango mkubwa wa moyo, na ndiyo kuimarika kwa hisia kwa ajili hiyo tunapaswa kutahadhari nayo (macho) na kuhifadhi tupu, ima ni kujilinda na uzinifu au kuhifadhi uchi, na wasionyeshe uzuri wao isipokua kwa wale walio ruhusiwa kama Aya iliyotangulia. Imethubutu katika Musnad ya Imam Ahmad kwamba Abu Hureira amepokea hadithi kutoka kwa Mtume (SAW) akisema: (Aina mbili za watu wa motono  na mmoja wao ni mwanamke avaae nguo nyepesi isiositiri na inaonyesha uchi).

Wanawake wema waliotangulia walikua wakijiheshimu na wakivaa hijabu na kumcha Mwenyezi Mungu, tazama kisa cha Uzushi, pindi Mama yetu Aisha hakumsemesha swahaba Swafuwan hata neno na hivyo ndivyo walivyo fika Madina. Na pindi walipoamrishwa kuvaa hijab waliitikia kwa haraka wito huo bila ya kuchelewa. Ummu salama asimulia akisema pindi ilpoteremka Neno lake Mwenyezi Mungu: "Wateremsha nguo zao". Wamefika wanawake wa kianswaar kama juu ya vichwa vyao kuna kurabu, na wakivaa vazi jeusi Mwenyezi Mungu mkubwa kwa kuitika wito wake na wito wa Mtume wake.
Imepokewa na Ummu Salama kua akisema mwanamke akimwambia Mtume (SAW) kua mimi ni mwanamke kurefusha vazi langu na natembea katika maeneo yenye uchafu? Akasema Mtume (SAW): [ itatwahirika baada yake]. Amesema kua mwanamke huyo anakusudia kuficha nguo zake pindi anapotembea kama iliyoada ya waarabu.  Wanawake wetu na mabanati wetu wakiachwa bila ya muongozo wa dini watafanya maovu na Mwenyezi Mungu kajalia kuwa wanaume ndio wasimamizi wao kutokana na upungufu wa akili na dini amabalo hilo Mtume (SAW)  anausia wanaume akisema:  [ Na kusieni kuwafanyia wema wake zenu kuweni ni wasiadizi wenu].
Ndugu Waislamu, tumeona khatari kubwa ya Fitna za Wanawake na athari mbaya katika jamii. Nijukumu lakila Muislamu kujitolea kubadilisha hali mbaya tunaoishi kwasasa katika jamii yetu. Ikiwa ni mkeo, mamako, bintiyako, binti wa muislamu mwenzako, wote nijukumu la kila muislamu kuwafundisha wanawke maadili na tabia njema. Tukifanya hivyo, kwahakika jamii yetu itabadilika na tutapata rehma za Allah (SW) pamoja na hifadhi yake kutokana na kila fitna. Namuomba Mwenyezi Mungu atulinde na fitna za wanawake, na awalinde wao na moto uumizao, Ewe Mwenyezi Mungu tupe mema hapa duniani na kesho akhera.

No comments:

Post a Comment

Twitter Bird Gadget