
Madhumuni ya blogu hii ni matatu: Kwanza:Kuelimishana sisi waislamu mambo yanayo tuhusu (uislamu) Pili:Kujulishana hitilafu zilizopo katika imani nyingine{ifahamike vizuri kuwa lengo sio kukashifu imani nyingine bali kuzitohoa hitilafu zilizopo katika imani hizo ili kuwa na upeo mkubwa wa uelewa utaowasaidia kutoshawishiwa au kutoritadishwa na makafiri (wasio waislamu)}. Tatu: Kuungana na waislamu wengine kwa kuweka makala au post zao hapa ili kusambaza ujumbe uliokusudiwa.
Wednesday, April 4, 2012
NASAHA - UNAPOKUWEPO KAZINI
Hivyo tutakuwa wizi wa fadhila kama hatutamshukuru Allah Subhaanahu Wata’aala kwa kutuwezesha kufanikisha azma yetu hii na pia kwa kutupa uwezo na afya /uzima wa kuweza kufanya kazi . Pia tutatakiwa kuzingatia yafuatayo wakati tupo kwenye hizi ajira zinazotupatia rizki zinazokwenda kwenye matumbo yetu , na ya ahli, watoto na wote wanaotutegemea kwani mwisho wa aya Allah (Subhaanahu Wata’aala) anatutanabahisha kwamba kutakuwa na kufufuliwa na kuulizwa kwa kila jambo mpaka hili la rizki inayoingia kwenye matumbo yetu. Kama hadithi ya Mtume
1 Mkumbuke Allah(Subhaanahu Wata’aala) na utawakkal kwake kila wakati na hasa unapokuwepo kazini.Unaweza kuleta dhikr na kumtaja huku unafanya kazi au kusoma Quraan kama umehifadhi ikiwezekana na hata kujikumbusha hadithi za Mtume
Tukifanya kazi vizuri ndipo tutakapopendwa na Allah (Subhaanahu Wata’aala) pamoja na Mtume wake
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment