Wednesday, April 4, 2012

Qur'an- Maana,Ubora na Fadhila Zake




Qur’aan tukufu ni maneno ya Allah aliyoteremshiwa Mtume Muhammad Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam na ikawa ni muujiza uliobaki milele wa kuonesha ukweli  na hoja yenye nguvu ya dini ya kiislamu 

Kutokana nayo waislamu, wanapata hukumu na muongozo wa maisha yao ya kila siku duniani na matarajio ya akhera na pia habari za umma zilizotangulia.

 

MAANA YA QUR’AAN

Asili ya neno Qur’aan linatokana na Qa-ra-a – kusoma na Al Qur-aan ni chenye kuunganishwa pamoja au chenye kusomwa

 

Ni maneno ya Allah Subhaanahu Wata’ala aliyoteremshiwa Mtume Muhammad Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam kupitia Malaika Jibreel ‘Alayhi Ssalaam yaliyohifadhiwa katika vitabu na ni  ibada  kubwa kuisoma kwake

Miongoni mwa majina na sifa za Qur’aan

 

MAELEZO

JINA/SIFA

 

MAELEZO

JINA/SIFA

 

Ponyo pekee au dawa

Ash-shifaa

9.

Maneno ya Allah

Kalaamullah

1.

Rehema kwa watu

Ar Rahmah

10

Mkusanyiko wa kurasa

Al Mus-haf

2.

Kheri pekee

Al Khayr

11

Kitabu pekee kisicho dosari

Al Kitaab

3.

Roho ya maisha

Ar-Ruuh

12

Kipambanuzi cha haki /batili

 Al Furqaan

4.

Chenye maelezo ya wazi

Al Bayaan

13

Mawaidha au ukumbusho

Adh Dhikr

5.

Muangaza

An-Nuur

14

Mshuko au Wahyi 

At Tanzeel

6.

Hoja pekee iliyowazi

 Al Burhaan

15

Kihukumu

Al Hukm

7.

Haki na ukweli

Al Haqq

16

Chenye hekima isiyo kikomo

Al Hikma

8.

Maelezo mazuri

Ahsanul Hadith

17

 

 

 

 

 

UBORA NA FADHILA ZAKE

Anasema Allah Subhanahu Wata,ala katika Qur’aan

 (إِنَّ الَّذِينَ يَتْلُونَ كِتَابَ اللَّهِ وَأَقَامُوا الصَّلاةَ وَأَنْفَقُوا مِمَّا رَزَقْنَاهُمْ سِرّاً وَعَلانِيَةً يَرْجُونَ تِجَارَةً لَنْ تَبُورَ) (فاطر:29)  .

Hakika wale wanaosoma kitabu cha Allah, wakasimamisha sala na wakatoa tulivyowaruzuku kwa siri na dhahiri watarajie bishara isiyokatika (Faatwir:29).

 

قال رسول الله صلى الله عليه وسلم :" ما اجتمع قومٌ في بيت من بيوت الله يتلون كتاب الله ويتدارسونه بينهم إلا نزلت عليهم السكينة وغشيتهم الرحمة وحفتهم الملائكة وذكرهم الله فيمن عنده ".

                                                                          رواه مسلم

Na anasema Mjumbe wa Allah Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam

Hawakusanyiki watu katika nyumba miongoni mwa nyumba za Allah  wanasoma kitabu cha Allah na wanafundishana baina yao  ila huteremka juu yao utulivu na hufunikwa na rehma na huzungukwa na Malaika na huwataja Allah mbele ya waliokuwemo

                                                                            Muslim

 

 

 وقال صلى الله عليه وسلم

  :" البيت الذي يُقرأُ فيه القرآن يتراءى لأهل السماء كما يتراءى الكواكب لأهل الأرض ".

Na amesema Mjumbe wa Allah Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam

“Nyumba inayosomwa Qur’aan inaonekana kwa waliokuwa mbinguni kama zinavyo onekana nyota kwa watu wa duniani”.

 

وقال صلى الله عليه وسلم :" أفضل عبادة أمتي قراءة القرآن " .

Na amesema Mjumbe wa Allah Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam

“Bora katika ibadah za umma wangu ni kusoma Qur’aan”

 

 وقال صلى الله عليه وسلم :" الذي ليس في جوفه شيء من القرآن كالبيت الخَرِب ".

Na amesema Mjumbe wa Allah Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam:

“Yule ambaye hana katika kifua chake chochote katika Qur’aan ni kama jumba lilo hamwa.”

 

وقال صلى الله عليه وسلم :" اقرءوا القرآن فإنّه يأتي يوم القيامة شفيعاً لأصحابه... "       رواه مسلم

Na amesema Mjumbe wa Allah Salla Allahu ‘Alayhi Wasallam:

“Someni Qur’aan hakika itakuja siku ya qiyama kuwaombea msamaha waliokuwa wanaisoma.           Muslim

وقال صلى الله عليه وسلم

 

الماهر بالقرآن مع السفرة الكرام البررة        رواه البخاري ومسلم.

                                     

 

Aliye mahiri katika Qur’aan anakuwa pamoja na Malaika walio wakarimu walio wema

                                                                                          

Bukhariy na Muslim


Abu 'AbdiRrahmaan









No comments:

Post a Comment

Twitter Bird Gadget